Na Fredy Mgunda,Iringa.
BARAZA la Vyama vya hiari na
Maendeleo ya Jamii (TACOSODE) limesema wananchi wamekuwa na uelewa kuhamasisha
bajeti kuwa na kipaumbele kwa changamoto zinazowakabili.
Hayo ameyasema Mkurugenzi wa
Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga wakati akizungumza semina ya kujadilia
jinsi gani ya kutatua changamoto zinazoikumba sekta ya afya iliyofanyika katika
ukumbu wa valentine Manispaa ya Iringa.
“Unajua zamani wananchi hata
viongozi wa sekta ya afya walikuwa wagumu kuelezea changamoto zinazowakabili
lakini saizi wananchi na viongozi wamekuwa na elimu ya kutosha juu ya kueleza
changamoto zilizopo katika sekta hiyo ndio maana vitu vingi vinaibuka muda huu”
alisema Kapinga
Kapinga alisema licha ya
serikali kufanya juhudi kutatua changamoto ili kuto huduma ya afya bora lakini
bado sekta hiyo inaendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo
zinakwamisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.
“Ukiangalia tafiti nyingi
zinaonyesha kuwa serikali imekuwa ikishindwa kuongeza bajeti ya sekta ya afya
ili kufikia asilimia 15 ya bajeti yote ya serikali kwa kuzingatia azimio la Abuja”
alisema Kapinga
Mkurugenzi wa Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga akizungumza jambo wakati wa semina iliyofanyika katika ukumbi wa valentine mkoani Iringa
Afisa mchechemzi wa mradi Abrahm Kimuli akiendelea kutoa elimu kwa wanasemina walikuwa wamehudhuria katika ukumbi wa valentine
Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye mijadala ya sekta ya afya na jinsi gani wanaweza kutatua changamoto zinazoweza kuikoa sekta ya afya hapa nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...