Na Fredy Mgunda,Iringa.

BARAZA la Vyama vya hiari na Maendeleo ya Jamii (TACOSODE) limesema wananchi wamekuwa na uelewa kuhamasisha bajeti kuwa na kipaumbele kwa changamoto zinazowakabili.

Hayo ameyasema Mkurugenzi wa Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga wakati akizungumza semina ya kujadilia jinsi gani ya kutatua changamoto zinazoikumba sekta ya afya iliyofanyika katika ukumbu wa valentine Manispaa ya Iringa.

“Unajua zamani wananchi hata viongozi wa sekta ya afya walikuwa wagumu kuelezea changamoto zinazowakabili lakini saizi wananchi na viongozi wamekuwa na elimu ya kutosha juu ya kueleza changamoto zilizopo katika sekta hiyo ndio maana vitu vingi vinaibuka muda huu” alisema Kapinga

Kapinga alisema licha ya serikali kufanya juhudi kutatua changamoto ili kuto huduma ya afya bora lakini bado sekta hiyo inaendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinakwamisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

“Ukiangalia tafiti nyingi zinaonyesha kuwa serikali imekuwa ikishindwa kuongeza bajeti ya sekta ya afya ili kufikia asilimia 15 ya bajeti yote ya serikali kwa kuzingatia azimio la Abuja” alisema Kapinga
 Mkurugenzi wa Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga akizungumza jambo wakati wa semina iliyofanyika katika ukumbi wa valentine mkoani Iringa
Afisa mchechemzi wa mradi Abrahm Kimuli akiendelea kutoa elimu kwa wanasemina walikuwa wamehudhuria katika ukumbi wa valentine
 Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye mijadala ya sekta ya afya na jinsi gani wanaweza kutatua changamoto zinazoweza kuikoa sekta ya afya hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...