Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Ndg. Geoffrey Mwambe amesema kwamba taarifa zilizotolewa na Mwandishi wa FT. John Aglionby kuhusu mazingira ya Uwekezaji Tanzania kuwa yanatishia wawekezaji si sahihi na yanalenga kupotosha ukweli kuhusu hali halisi kuhusu Uwekezaji Tanzania.

Mwandishi huyo wa Financial Times ametoa maelezo ambayo amesema yametolewa na Muwekezaji Aliko Dangote maelezo ambayo yamelenga kusukuma Agenda yake ambayo haijulikani na yenye lengo la kupotosha sera za uwekezaji na kuwaogopesha wawekezaji ambao wameendelea kuiamini Tanzania na kuwekeza mitaji yao mikubwa hapa nchini.

Hatuamini kuwa Ndugu Dangote anaweza kuwa msemaji wa kuhusiana na sekta ya madini kwa hapa nchini. Amewekeza kwenye sekta ya viwanda na serikali imekuwa mstari wa mbele kusikiliza na kuyafanyia kazi maoni ya mfanyabiashara huyo ili kuweza kuboresha mazingira yetu ya uwekezaji hapa nchini. Serikali yetu imejidhatiti katika kuboresha mazingira ya uwekezaji na imedhamiria kuhakisha uwekezaji huo unakuwa na faida kwa watanzania nan chi kwa ujumla.

Tunaamini kuwa kuna umuhimu wa kuhakikisha maelezo yanakuwa na pande mbili ili kuondoa utata utaojitokeza wa maelezo ambayo yanaweza kuathiri na kusababisha utata kwa wafanyabiashara walioiamini Tanzania kama sehemu yao ya kufanya uwekezaji. 

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...