TIMU ya Taifa ya mpira wa wavu imepanda kwa nafasi 19 kwa timu za wanaume na wanawake na kuanza kufufua matumaini ya mchezo huo kufanya vizuri  kimataifa zaidi baada ya mwanga na kwenda mbali zaidi.


Tanzania imesogea kwenye viwango hivyo kutoka nafasi ya 137 hadi 118 kwa wanaume huku kwa wanawake ikitoka nafasi ya 115 hadi 97, kwa Afrika Mashariki ni Kenya inayoongoza kwa wanaume ikiwa nafasi ya 33, Uganda 55, Burundi 97, Rwanda 114.

Nasoro Sharif ambaye ni kocha na mchezaji wa timu ya taifa ya wavu amesema kuwa  jitihada ndizozimewafikisha hapo na hawawezi kuacha kujituma uwanjani na katika michezo ijayo pia   kinachotakiwa kwa sasa ni kuendelea kuupigania mchezo huo ili tusogee zaidi kwenye viwango hivyo sawa na wenzetu wa Kenya.


“Uongozi mpya unaweza kutusaidia kwa kiasi kikubwa maana unonekana kuja na mambo mengi mazuri, Tanzania imekosa michezo mingi ya kimataifa nadhani itakiwa tuwe na michezo mingi ili itusaidie kupanda," alisema mchezaji huyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...