Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe ametembelea Mradi wa Maji
Longido, mkoani Arusha kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wake, kwa lengo la
kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kumaliza kero ya maji kwa wakazi wa Longido.
Mhandisi Kamwelwe ametembelea mradi huo na kuridhishwa na hatua iliyofikiwa hadi
sasa, ambao Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliweka jiwe la msingi mnamo Oktoba 21,
2017 na kuagiza ukamilike kwa wakati na kuanza kuhudumia wakazi wa Mji wa Longido
na Kijiji cha Engikaret.
‘‘Serikali imedhamiria kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa majisafi na salama
Wilayani Longido kwa kutekeleza mradi huu mkubwa wa maji kutoka katika chanzo cha
maji cha Mto Simba kilichopo Wilaya ya Siha, mkoani Kilimanjaro umbali wa kilomita 64
mpaka Longido.’’
‘‘Nimeridhishwa na hatua ya utekelezaji wa mradi huu unaosimamiwa na Mamlaka ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira ya Mji wa Arusha (AUWSA) na utaigharimu Serikali kiasi
cha Sh. bilioni 15.8 ambazo ni fedha za ndani’’, alisema Waziri Kamwelwe.
Mradi huo unategemea kuzalisha lita 2,160,000 kwa siku wakati mahitaji halisi kwa sasa
ni lita 1,462,000, na unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji kwa asilimia 100 (sawa
na wakazi 26,145 kwa sasa) wa Mji wa Longido kufikia 2024 na Kijiji cha Engikaret
chenye wakazi wapatao 1,294.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akikagua chanzo cha
maji cha Mto Simba, wilayani Siha.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akiangalia kazi ya
uunganishaji wa mabomba yanayolazwa kwa ajili ya mradi wa Longido, Siha,
mkoani Kilimanjaro.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe na Mkurugenzi wa
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (AUWSA), Mhandisi Ruth Koya
Kilimanjaro, wakiwa mbele ya tenki la maji Longido.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza na
wakazi wa Kijiji cha Engikaret, ambao ni miongoni mwa watakaonufaika na mradi
wa maji wa Longido, mkoani Arusha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...