Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga,  Juma Abed akizungumza na waandishi habari mara baada ya kuahirisha kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika mapema wiki hii kikiwa na lengo la kujadili mikakati ya kimaendeleo ya Mkuranga.


Baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Mkuranga limeitaka wakala wa Barabara mijini na vijijini (Tarura) kushirikiana na halmashauri na viongozi wa ngazi za chini katika kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo husika.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya baraza la  Madiwani la halmashauri ya  mkuranga mwenyekiti wa baraza hilo, Juma Abed amesema tarura imekua ikifanya kazi zake bila kuwashirikisha madiwani hali ambayo inasababisha utendaji na utekelezaji wa miradi ya barabara kutotekelezeka kwa wakati.

Aidha Abed amesema kuwa miradi ya ujenzi wa miundombinu  ya barabara ijengwe imara na kuachana na biashara ya ujenzi wa kila mwaka.
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Mkuranga, Mshamu Munde akizungumza juu ya mikakati ya Halmashauri hiyo ikiwemo kuboresha miundo mbinu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga, Juma Abed akiwa katika picha ya pamoja madiwani, watendaji wa Halmashauri.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...