Mkuu
wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe amewataka wananchi wa Kata ya
Kwamgwe kuendelea kujitoa kikamilifu katika kuchangia shughuli za
kijamii ili kuendana na kasi ya rais Dkt. John Magufuli katika kuleta
maendeleo endelevu.
Akizungumza
na wakazi wa Kata ya Kwamgwe wakati akikabidhiwa zahanati iliyojengwa
kwa hisani ya shirika la maendeleo la World Vision Tanzania, mkuu wa
wilaya aliwaomba wananchi waendelee na moyo wa kujitolea katika
kuchangia kazi za maendeleo ili kijiji kiweze kujikwamua.
"Nawaomba
ndugu zangu, sisi wote ni wanaKwamngwe, lazima tuamue kuchangua mambo
muhimu matatu, kutambaa, kutembea au kukimbia. Jambo la msingi ni lazima
tuwe katika mwendo, tuendelee kujitoa tuzidi kuleta maendeleo kijijini
kwetu," alisema Gondwe.
Awali
akikabidhi mradi huo wa zahanati hiyo, Mwezeshaji wa mradi Mkumburu
ADP, Humphrey Bernard aliwashukuru wananchi wa kata ya Kwamgwe kwa
kuweza kujitoa kufanikisha ujenzi wa jengo la zahanati.
Wakati
huo huo, Mkuu wa wilaya Handeni aliweza kutembelea ujenzi wa kituo cha
afya cha Michungwani, Segera ambapo ujenzi wake unaanza hivi karibuni
kwa nguvu za wananchi kupitia kampeni ya mkuu huyo ya kuongeza zahanati
na madarasa.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe akiongea na wananchi wa Kata ya Kwamgwe wakati akikabidhiwa zahanati iliyojengwa kwa hisani ya shirika la maendeleo la World Vision Tanzania kwa kushirikiana na nguvu za wananchi, mkuu wa wilaya aliwaomba wananchi waendelee na moyo wa kujitokea katika kuchangia kazi za maendeleo ili kijiji kiweze kujikwamua kimaendeleo. PICHA NA KAJUNASON/MMG - HANDENI, TANGA.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Handeni, William Makufwe akitoa ufafanuzi
jinsi wananchi walivyoweza kujitoa ujenzi wa zahanati.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe akimsaidia Diwani wa Kata ya Kwamgwe, Sharifa Abebe alipokuwa akitoa machozi ya shukrani kwa shirika la maendeleo la World Vision Tanzania kwa kuweza kushirikiana na wananchi kuwajengea jengo la zahanati lililoweza kugharimu shilingi milioni 190 ambapo wao World Vision Tanzania waliweza kutoa Milioni 100 na wao wananchi waliweza kujitoa kwa nguvu zao kwa thamani ya milioni 90. Hafla hiyo ilifanyika katika Kata ya Kwamgwe ambapo ndipo jengo hilo lilipojegwa.
Mwezeshaji wa mradi Mkumburu ADP wa World Vision Tanzania, Humphrey Bernard akisoma risala ya mradi wa ujenzi wa zahanati iliyojengwa katika Kata ya Kwamgwe ambapo aliwashukuru wananchi wa kata ya Kwamgwe kwa kuweza kujitoa kufanikisha ujenzi wa jengo la zahanati.
Mkuu wilaya akipata maelezo machache kutoka kwa wananchi waliitikia wito wa kuchangia maendeleo kwa kuchimba msingi wa zahanati ya Migombani, Michungwani - Segera.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...