Na Shamimu Nyaki –WHUSM.
Wizara
ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo imeandaa Kampeni ya “Uzalendo na
Utaifa” inayotarajiwa kuzinduliwa Disemba nane mwaka huu Mjini Dodoma na
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
lengo ikiwa ni kurejesha hali ya Uzalendo na Utaifa katika kutatua
changamoto zilizojitokeza na zitakazojitokeza katika Taifa letu.
Akizungumza
na Wakuu wa Taasisi za Serikali jana Jijini Dar es Salaam Waziri wa
Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amesema
kuwa Kampeni hiyo inadhamiria kuwakumbusha watanzania Utamaduni wetu na
Uzalendo uliokuepo miongoni mwa Watanzania ambao ulileta heshima kubwa
ndani na nje ya nchi.
“Kampeni
hii ina lengo la kurudisha Uzalendo tuliokuwa nao Watanzania katika
kuheshimu mali za Umma, kuogopa rushwa,ubaguzi wa
kidini,kikabila,kiitikadi na kikanda ambavyo vilianza kupotea,lakini
Serikali ya awamu ya Tano imeanza kurudisha hivyo sisi kama watanzania
tunapaswa kuunga mkono jitihada hizi”Alisema Dkt. Mwakyembe.
Aidha
Dkt. Mwakyembe ameeleza kuwa Kampeni hiyo inatarajiwa kuleta matokeo
chanya ikiwemo kurejesha na kuimarisha moyo wa Uzalendo na Utaifa kwa
Watanzania hususan vijana na watoto umuhimu wa kuipenda na kuithamini
nchi yao pamoja na kuimarisha umoja upendo na mshikamano wa kitaifa.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Wakuu wa Taasisi za Serikali kutoka Kituo cha
Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geofrey Mwambe amesema Taasisi za Serikali
zinaunga mkono Kampeni hiyo kwani itasaidia watanzania wengi kuelewa
historia na Utamaduni ya nchi yao na kuitilia maanani popote
watakapokuwa.
Kampeni
hiyo yenye kauli mbiu “Nchi Yangu Kwanza” itakuwa ni endelevu na
inatarajiwa kufanyika kila mwezi Oktoba kama sehemu ya maadhimisho ya
kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
akizungumza jana Jijini Dar es Salaam na Wakuu wa Taasisi za Serikali
kuhusu Kampeni ya Uzalendo na Utaifa inayotarajiwa kuzindiliwa mwezi
ujao Mjini Dodoma.
Mwenyekiti
wa Wakuu wa Taasisi za Serikali Bw. Geofrey Mwambe kutoka Kituo cha
Uwekezaji Tanzania (TIC) (aliyesimama )akizungumza wakati wa kikao na
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison
Mwakyembe pamoja na Wakuu hao kuhusu Kampeni ya Uzalendo na Utaifa
inayotarajiwa kuzindiliwa mwezi ujao Mjini Dodoma.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas
akiwaonyesha Wakuu wa Taasisi za Serikali Jarida la Nchi Yetu
linaloelezea mafanikio ya miaka miwili ya Serikali ya awamu ya Tano
lililondaliwa na Idara yake kwa kushirikiana na Taasisi hizo jana Jijini
Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...