Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakijiandaa kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro.


Na Dixon Busagaga, Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MPANDA milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal raia wa Ureno na wenzake wawili wameanza safari ya siku tano ,kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia lango la Kilema ikiwa ni aina mpya ya utalii iliyoanza kushika kasi katika hifadhi hiyo.

Hatua hiyo inatokana na jitihada za shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kueendelea kupanua wigo wa vivutio katika Hifadhi zake 16,kwa kuanzisha aina mpya ya bidhaa za utalii ili kushindana na nchi nyingine duniani katika uuzaji wa safari kwa watalii.

Miongoni mwa bidhaa hizo ni pamoja na zile zilizoanzishwa katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimajaro (KINAPA) ya kuzunguka mlima kwa kutumia Parachuti pamoja na kupanda Mlima kwa kutumia Baiskeli, utalii ambao umeanza kushika kasi.

Juanito Oiarzabal ambaye tayari ameweka rekodi nyingi duniani na kuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu kijulikanacho kama World Guinness Book amepanda mlima Kilimanjaro na wenzake wawili ,Eduardo Pascuaz na Ramon Abecia kwa kutumia Baiskeli .

Mkurugenzi wa Utali wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA ) Ibrahim Musa amesema Oiarzabal atakuwa Mreno wa kwanza kuweka rekodi ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia baiskeli na kwamba aina hi ya utalii na rafiki kwa mazingira ya Hifadhi.

Mkurugenzi wa kampuni ya Safari Bike Africa inayoratibu wa changamoto hii a kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli,Mario Martos amesema hatua hii ni mwanzo wa kufungua aina hii ya utali katika Hifadhi za Taifa za Arusha na Saadan.

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro limeweka utaratibu wa kufanya vipimo kwa wapandaji wa Mlima kwa wanao tumia Baiskeli pia kabla ya kuanza safari ya kuelekea kileleni.

Juanito na wenzake wawili wameianza safari ya siku tano ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia baiskeli wakipita lango la Kilema ambapo wanatarajia kupita katika Kilele cha Mawenzi kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea kilele cha Uhuru.
Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu wa safari hiyo ambaye pia ni mkurugenzi wa kampuni ya Safari Bike Africa ,Mario Martos pamoja na waongoza watalii ,Ally Chuwa na Elvas Mlengwa kabla ya kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro
Eduardo Pascuaz akifunga kofia ngumu kabla ya safari ya kuelekea Kilele cha Uhuru kuanza.
Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakijiandaa kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...