Meneja Amana za wateja binafsi NBC
Dorothea Mabonye na Meneja Mikopo ya wateja binafsi Mtenya Cheya wakimpigi
mteja aliyeshinda katika droo ya kwanza ya kampeni ya Akaunti ya Malengo ijulikanayo
kama Malengo na Kirikuu, aliyejishindia zawadi ya shillingi milioni moja. Wanao
shuhudia tukio hilo Kutoka kushoto. Meneja masoko wa NBC Alina Maria Kimaryo,
na Msimamizi kutoka Bodi ya Bahati Nasibu ya Taifa Bakari Maggid. NBC
iliendesha droo ya kwanza ambayo ilitoa jumla ya washindi 12 walijishindia
shillingi milioni moja kila mmoja.
Meneja masoko wa NBC Alina Maria Kimaryo (katikati)
akionyesha vipeperushi vya kampeni ya akaunti ya malengo ijulikanayo kama
Malengo na Kirikuu kwenye droo ya kwanza. Kushoto ni Meneja mwandamizi wa
mahusiano ya Umma William Kallaghe na kulia ni Meneja Amana za wateja binafsi
NBC Dorothea Mabonye. NBC iliendesha droo ya kwanza ambayo ilitoa jumla ya
washindi 12 walijishindia shillingi milioni moja kila mmoja.
Meneja masoko wa NBC Alina Maria
Kimaryo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa droo ya
kwanza ya kampeni ya akaunti ya Malengo ijulikanayo kama Malengo na Kirikuu.
Katika droo hiyo jumla ya washindi 12 walijishindia shillingi milioni moja kila
mmoja. Wanao shuhudia ni Meneja Amana za wateja binafsi NBC Dorothea Mabonye
(kati kati) na Meneja Mikopo ya wateja binafsi NBC Mtenya Cheya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...