Magari ya ya Jeshi la zimamoto yakiwa yamefika eneo la tukio,katika jengo la Ofisi za Clouds Media Group lililopo Mikocheni jijini Dar, kukabiliana na moto uliozuka mapema leo kwenye moja chumba cha ofisi na kusababisha baadhi ya vifaa kuungua na kuharibika kabisa,aidha mpaka sasa Globu ya jamii haijaelezwa haswa chanzo cha moto ni nini.Hivyo Tunaendelea kufuatilia na kupata taarifa kamili.
Sehemu ya jengo la Ofisi za Clouds Media Group kama lionekanavyo pichani huku shughuli za uzimaji moto huo ukiendelea .
Mmoja wa Askari wa jeshi la Zimamoto akiendelea kuudhibiti moto uliokuwa umezuka ndani ya moja ya Ofisi za jengo hilo
Baadhi ya Wafanyakazi wa Clouds Media Group pamoja na baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wa Clouds wakiwa nje ya jengo hilo wakifuatilia tukio la uzimaji moto uliozuka katika jengo hilo mapema leo,Mikocheni jijini Dar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...