Magari ya ya Jeshi la zimamoto yakiwa yamefika eneo la tukio,katika jengo la Ofisi za Clouds Media Group lililopo Mikocheni jijini Dar, kukabiliana na moto uliozuka mapema leo kwenye moja chumba cha ofisi na kusababisha baadhi ya vifaa kuungua na kuharibika kabisa,aidha mpaka sasa Globu ya jamii haijaelezwa haswa chanzo cha moto ni nini.Hivyo Tunaendelea kufuatilia na kupata taarifa kamili.
 Sehemu ya jengo la Ofisi za Clouds Media Group kama lionekanavyo pichani huku shughuli za uzimaji moto huo ukiendelea .
  Mmoja wa Askari wa jeshi la Zimamoto  akiendelea kuudhibiti  moto uliokuwa umezuka ndani ya moja ya Ofisi za jengo hilo
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Clouds Media Group pamoja na baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wa Clouds wakiwa nje ya jengo hilo wakifuatilia tukio la uzimaji moto uliozuka katika jengo hilo mapema leo,Mikocheni jijini Dar.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...