Mamlaka ya Vitambuisho vya Taifa (NIDA) inaendelea na zoezi la Usajili na Utambuzi wa watu mkoani Mbeya ambapo wananchi wengi wamejitokeza ambapo kwa sasa usajili unaoendelea niwa mkupuo (mass registration) ambapo wananchi wanakusanyika kwenye mitaa na vijiji wanakoishi kusajiliwa ambapo Usajili huo unahusisha ujazaji fomu, uchukuaji alama za vidole picha na saini ya kielektroniki. 

Akitoa elimu kwa umma kuhusu taratibu za Usajili mwakilishi wa kitengo cha Mawasiliano NIDA Bw. Deodatus Alexander Mchaki amesema zoezi hilo ni fursa ya kipekee kwa wananchi kutambuliwa na kusajiliwa.

Amesisitiza zoezi la usajili ni Bure na wananchi hawatakiwa kutozwa gharama zozote Ili kusajiliwa mwananchi ni lazima afike na nakala (photocopy) ya nyaraka/viambatisho vifuatavyo kuthibitisha Umri, Uraia na Makazi yake ikiwemo cheti cha kuzaliwa, Passport (Pasi ya kusafiria), Kadi ya kupigia kura, leseni ya udereva, ID ya Mzanzibar mkazi, TIN, Pasi ya kusafiria na vyeti vya elimu.
Wananchi wa Kata ya Mwakidete mtaa wa Mwakidete mkoani Mbeya wakiendelea na Usajili Vitambulisho vya Taifa.
Mmoja wa wananchi wa Mtaa wa Mwakidete akiweka saini kwenye mashine maalumu ya uchukuliaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki.
Wanaoonekana kwenye picha ni Baadhi ya Maafisa Usajili wa NIDA wakiendelea na zoezi la kuwasajili wananchi wa Kata ya Mwakidete mkoani Mbeya. Kushoto ni Afisa Usajili Wilaya ya Mbeya Bi. Alavuya Ntalimwa akitabasamu jambo na wananchi wa Mtaa wa Mwakidete.
Mwananchi akichukuliwa alama za Vidole na afisa Usajili wa NIDA wakati zoezi la kuwasajili wanannchi likiendelea. 
Msururu wa wananchi wa Mtaa wa Mwakidete wakisubiri huduma ya usajili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...