KAMATI ya Bunge ya Katiba na Sheria imepongeza namna mifuko ya hifadhi ya jamii ya NSSF na PPF inavyotekeleza mradi wa pamoja wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unaofahamika kama Mkulazi huku ikitoa wito kwa wadau hao kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kwa wakati ili kulinusuru taifa na uhaba wa bidhaa hiyo.

Mwisho mwa wiki kamati hiyo ilitembelea mradi huo unaotekelezwa katika gereza la Mbigiri, lililopo Dakawa mkoani Morogoro kupitia kampuni Hodhi ya Mkulazi Holding inayoshirikiana na Jeshi la Magereza nchini.

"Baada ya kusikiliza mpango mikakati na kisha kutembelea shamba husika kiukweli kamati yetu imeridhishwa sana na jinsi wadau hawa wanavyotekeleza mradi huu. Ni wazi kuwa walifanya utafiti wa kutosha kabla na matunda yake kiukweli yameanza kuonekana kikubwa tu tunachowaomba wamalize mradi huu kwa wakati .'' alisisitiza  Mwenyekiti wa kamati hiyo Bw Mohamedi Mchengelwa.

Aidha, wajumbe wa kamati hiyo walionyesha kuridhiswa zaidi na namna mradi huo unavyohusisha wananchi walio jirani na maeneo ya mradi ambao mbali na kupata ajira za moja kwa moja pia wamepatiwa fursa ya kulima miwa ili kukiuzia kiwanda hicho, hatua waliyosema kuwa itapunguza tatizo la ajira na kuongeza kipato cha wananchi.

"Kingine kikubwa zaidi kwa wadau hawa ni kuhakikisha kuwa mradi huu hauishii kwenye kuzalisha sukari tu bali pia bidhaa zitokanazo na mabaki ya malighafi za miwa ikiwemo ethanol, vyakula vya mifugo pamoja na uzalishaji wa nishati umeme,'' alisema mjumbe Selemani Zedi huku akiungwa mkono na wenzie akiwemo Mbunge wa Wawi Ali Salehe.
 Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  (wa tatu kulia) akiwaongoza baadhi ya wajumbe wa kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria  kukagua shamba hilo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria Bw Mohamedi Mchengelwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba kubwa la miwa lililopo katika gereza la Mbigiri lililopo Dakawa mkoani Morogoro ambalo ni sehemu ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha sukari kinachojengwa kwa ubia kati ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF, PPF na jeshi la Magereza nchini.
 Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba hilo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mkulazi ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba hilo. Kwa mujibu wa Prof. Kahyarara hadi kufikia mwishoni mwa mwaka ujao mradi huo utakuwa tayari umeanza kuzalisha sukari pamoja na baadhi ya bidhaa ambatanishi ikiwemo uzalishaji wa umeme.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...