Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira
na Walemavu), Jenista Mhagama akimkabidhi cheti cha ushiriki Tuzo za
Mwajiri Bora 2017 (EYA), Mkuu wa Rasilimali watu wa Exim Bank Tanzania,
Mr Fredrick Kanga kwenye hafla ya utoaji tuzo hizo iliyofanyika jijini
Dar es Salaam jana usiku. Exim Bank Tanzania imeshinda tuzo ya ushindi
wa jumla wa mwajiri bora wa ndani ya nchi.
Mkuu
wa Rasilimali watu wa Exim Bank Tanzania, Mr Fredrick Kanga akipokea
tuzo ya ushindi wa jumla wa mwajiri bora wa ndani ya nchi jana usiku
katika halfa ya utoaji tuzo hizo kutoka chama cha waajiri Tanzania (ATE)
Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Rasilimali watu wa Exim Bank Tanzania, Mr Fredrick Kanga pamoja na Mr Stanely Kafu, Mkuu wa idara ya masoko wa benki hiyo wakipiga picha na baadhi ya wafanyakazi katika halfa ya utoaji tuzo hizo kutoka chama cha waajiri Tanzania (ATE) Dar es Salaam jana ambapo Exim Bank Tanzania imeshinda tuzo ya ushindi wa jumla wa mwajiri bora wa ndani ya nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...