Kilimanjaro Stars, ilicheza mchezo wa kwanza dhidi ya Libya Jumapili Desemba 3, mwaka huu kwenye Uwanja wa Kenyatta na matokeo yakawa sare tasa katika mfululizo wa mechi za michuano ya Cecafa.
Katika mazoezi yaliyofanyika Uwanja wa Machakos Academy leo asubuhi, Kocha Ninje ameanza kufanyia kazi namna ya kukaba wakati mpira unapokuwa kwa adui au timu inapopoteza mpira.
Baada ya mazoezi hayo Kocha Ninje ameoneshwa kufurahishwa na namna wachezaji walivyoelewa na kufanya kile alichowaelekeza kukifanya ambapo amesema inaonesha dalili nzuri ya kumaliza tatizo hilo lililoonekana kwenye mchezo wa kwanza na Libya.
Katika mazoezi hayo pia walifanya mazoezi ya namna ya kufanya mashambulizi na kupandisha timu.
Kesho wataendelea tena na mazoezi kujiandaa na mchezo unaofuata utakaochezwa Alhamis kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos dhidi ya timu ya Taifa ya Zanzibar.
Kilimanjaro Stars ipo kundi A pamoja na timu za Rwanda, Zanzibar, Libya na wenyeji Kenya ambapo kabla ya michezo ya leo katika kundi hilo – Harambee Stars inaongoza kwa kupata pointi 3 katika mchezo wa mwanzo, wakifuatiwa na Libya na Kilimanjaro Stars wenye pointi 1 kila mmoja wakati Zanzibar na Rwanda wakiwa hawana pointi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...