MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita ameondoka Jijini hapa jana jioni kuelekea Addis Ababa, kuhudhuria mkutano wa kujadili changamoto zinazo wakabili viongozi wa serikali za mitaa.

Mkutano huo wa siku tatu umeandaliwa na Umoja wa Mataifa ambapo unalengo la kujadili na kutoa majibu ya changamoto ambazo wanakutana nazo viongozi wa serikali za mitaa wakiwepo Mameya wote.

Miongoni mwa changamoto ambazo zitajadiliwa katika mkutamo huo pamoja na mambo mengine ni suala la bajeti katika halmashauri na ukusaji wa mapato.Mbali na Mameya ,mkutano huo pia utahudhuriwa na viongozi wengine wa serikali za mitaa kutoka Nchi mbalimbali.

Aidha Meya Mwita atazungumza na mkutano huo kuelezea changamoto zilizopo katika jiji la Dar es Salaam , namna ambavyo kwa asilimia kadhaa wameweza kuzitatua.Aidha katika mkutano huo ataeleza pia mafanikio yaliyopo katika jiji la Dar es Salaam kupitia sekta mbalimbali za Maendeleo.

” Katika mkutano huo hatuta kuwa jiji la Dar es Salaam pekee ,ni Nchi mbalimbali Duniani zitakuwepo, tutajadili changamoto zinazo tukabili kwenye halmshauri zetu, mafanikio,lakini pia kujengeana uwezo kwenye utendaji kazi” alisema Meya Mwita.

Imetolewa leo Desemba 11

Na Christina Mwagala , Afisa Habari Ofisi ya Mstahiki Meya wa jiji

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...