Kampuni ya Mohammed Enterprises (MeTL Group) imeshinda tuzo nne za
Mwajiri Bora wa Mwaka 2017 (EYA) zinazotolewa na Chama Cha Waajiri
Tanzania (ATE), katika hafla ya iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani
City Jijini Dar es Salaam. MeTL imeshinda tuzo hizo kupitia kampuni zake
tanzu ambazo ni Mo Assurance Limited iliyoshinda kipengele cha Tuzo ya
Kampuni Ndogo, 21st Century Holding Limited imeshinda nafasi ya pili ya
Tuzo ya Mwajiri Bora wa Ndani na Star Oil Tanzania Limited imeshinda
tuzo mbili, Tuzo ya Kampuni ya Kati na nafasi ya tatu ya Tuzo ya Mwajiri
Bora wa Ndani. Ushindi huo wa tuzo nne, umeiwezesha MeTL Group kuwa
moja ya kampuni nne ambazo zimeshinda tuzo nyingi za ATE 2017, na kuwa
kampuni ya kizalendo ambayo imeshinda tuzo nyingi kuliko kampuni zingine
ambazo zimeshiriki katika tuzo hizo. Kutoka
kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya Royal
Soap, Jackline Mbaga, Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya
Star Oil Tanzania Limited , Ester Dotto, Meneja Mkuu wa Mo Assurance
Limited, Kura Bonniface, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Mohammed
Enterprises, Hassan Dewji, Meneja Mauzo na Mkuu wa kitengo cha
Rasilimali Watu wa kampuni ya 21st Century Holding Limited, David
Mziray, Ofisa wa kitengo cha Rasilimali Watu wa Mohammed Enterprises,
Jessica Julius, Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya 21st
Century Textiles, Godfrey Ndimbo na Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu
wa kampuni ya 21st Century Food and Packaging, Anna Zongo wakiwa na tuzo
nne ambazo wameshinda kwenye tuzo za ATE 2017.
Akizungumza kuhusu ushindi huo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa MeTL Group, Hassan Dewji, alisema wamefurahishwa na ushindi huo, lakini pia unaonyesha jinsi gani kampuni inafanya vizuri katika soko la hapa nchini. "Tuna furaha kushiriki kwenye tuzo za ATE 2017 na tuna furaha kushinda tuzo nne, naamini tumekuwa moja ya kampuni tano ambazo zimeshinda tuzo nyingi. Nafikiri sisi ni moja ya kampuni kubwa nchini na tunaendelea kukua na kugusa maisha ya watu wengi kila siku, ushindi kama huu utuwezesha kuongeza juhudi zaidi," alisema Dewji.
Akizungumza kuhusu ushindi huo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa MeTL Group, Hassan Dewji, alisema wamefurahishwa na ushindi huo, lakini pia unaonyesha jinsi gani kampuni inafanya vizuri katika soko la hapa nchini. "Tuna furaha kushiriki kwenye tuzo za ATE 2017 na tuna furaha kushinda tuzo nne, naamini tumekuwa moja ya kampuni tano ambazo zimeshinda tuzo nyingi. Nafikiri sisi ni moja ya kampuni kubwa nchini na tunaendelea kukua na kugusa maisha ya watu wengi kila siku, ushindi kama huu utuwezesha kuongeza juhudi zaidi," alisema Dewji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...