Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Rais Dkt Ali Mohamed Shein akimpongeza Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Bw.Kheri James mara baada ya kushinda katika uchaguzi wa jumuiya hiyo uliofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Chuo Cha Mipango mjini Dodoma wa pili kutoka kulia anayeangalia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Bi. Tabia Mwita.PICHA NA MICHUZI JR DODOMA.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Rais Dkt Ali Mohamed Shein akimpongeza Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Bi. Tabia Mwita baada ya ushindi wake katikati anayeshuhudia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Bw. Kheri Denis James akiwa amebebwa na baadhi ya Wajumbe mara baada ya kutajwa kuwa ndiye Mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo kwa miaka mitano
Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu na Mkutano mkuu wa UVCCM wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutangazwa washindi katika mkutano huo.
Mara baada ya kutangazwa tu kuwa ndiye Mwenyekiti Mpya wa Jumuiya ya umoja wa Vijana (UVCCM),Kher Denis James,kwa furaha kubwa iliyokwenda mpaka kwa Wajumbe wenzake,ilibidi zitumike nguvu za ziada kupunguza vurugu za shangwe zilizotarajiwa kutokea ukumbini hapo,kama uonavyo Mwenyekiti akiwa katika mikono salama ya utuliu akielekezwa kwenda jukwaa kuu.
Makamu Mwenyekiti wa UVCCM aliyemaliza muda wake Mh. Mboni Mhita akimpongeza Makamu Mwenyekiti mpya Bi. Tabia Mwita.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Mh. Kassim Majaliwa pichani kushoto akitazama tukio la pongezi kutoka Makamu Mwenyekiti wa UVCCM aliyemaliza muda wake Mh. Mboni Mhita akimpongeza Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Bw. Kheri James.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...