Na Wankyo Gati,Arusha

Naibu waziri wa mawasiliano na uchukuzi Afashasta Nditie amezindua Mkutano mkuu wa kujadili mfumo wa Anuani za makazi uliofanyika mkoani Arusha ambao umewakutanisha wadau mbali mbali wa mawasiliano kutoka nchi za Africa .

Akizungumza na wadu hao Naibu waziri Nditie amesema kuwa mfumo huo kwa hapa nchini upo vizuri na anaamini kuwa mamalaka husika ipo makini katika kukamilisha hatua iliyobaki ambayo itaifanya Tanzania kufika mbali.

Aliongeza kuwa mbali na jitihada mbalimbali zinazofanyika kuweza kufikia kila moja lakini bado kuna changamoto mablimbali za kuwepo na mitaa mingi isiyokuwa na majina ili kuweza kurahisisha huduma ya posta mlangonii.

Kwa upande wake Kaimu Posta mkuu wa shirika la Posta Tanzania Hassani Mwang’ombe amesema kuwa hivi sasa wako katika mpango wa huduma ya posta mlangoni ili kuweza kurahisisha barua zote kumfikia kila mmoja mwananchi mahali anakoishi ili kuweza kupata mawasiliano.

Hata hivyo amesema kuwa watanzania watajiskia vizuri na kuona furaha pindi watakapo ona huduma ya posta inawafikia mpaka milangoni mwao kwani siwananchi wote wanaweza kumudu kwenda mahli paliko huduma ya posta ili kuweza kuwasaidia maelfu ya wakazi walio wengi.

Kwa upande wake katibu mkuu wa Papu Younoss Djibrine alisema kuwa nimwanzo mzuri wa na njia nzuri kwa nchi ya Tanzania kuweza kuanza huduma hii ya anuani na majina ya mtaa ambapo hata united nation nihaki ya kila mmoja kuweza kupata utambuzi wanakoishi lli kuweza kuwafuikia kirahisi zaidi.

Aliongeza kuwa nchi nyingi za afrika zinachangamoto mbalimbali kiwemo kukosa anuiani za makazi yao hali ambayo kuwafikia inakuwa vigumu sana lakini kuna haja za makusudi kuweza nchi husika kuweza kuanzisha utaratibu huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...