Naibu Waziri wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya ametembelea maonesho ya pili ya Viwanda vya Tanzania na kujionea uzalishaji wa bidhaa mbalimbali za viwanda vya Tanzania.
 Pia Naibu waziri amehudhuria mkutano wa wafanyabiashara wa Viwanda vya nchini uliojadili changamoto mbalimbali za uwekezaji na ufanyaji biashara nchini na kuwahakikishia wawekezaji wote wakubwa na wadogo kushirikiana na serikali katika kusema wapi wanakwamishwa ili juhudi za haraka zifanyike pale mwekezaji anapopata tatizo.
 Naibu Waziri amesema serikali inatambua umuhimu wao katika nchi hii na kuwaomba kufanya kazi kwa bidii na tija pia kulipa kodi ili kusaidia haraka maendeleo ya nchi.
Aidha Mhe. Waziri amezungumza na Waandishi wa habari na kueleza jinsi alivyojionea maonesho haya ambayo yamekuwa mfano kwa nchi yetu kwa kuwaleta pamoja wafanyabiashara na wawekezaji wote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...