Na Mwandishi Maalum
MKURUGENZI wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Kailima Ramadhani alisema chama cha siasa kutangaza kugomea kushiriki uchaguzi hakuwezi kuifanya tume ihahirishe uchaguzi kwani tume haiko kumshawishi mtu au chama kushiriki uchaguzi.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Ramadhani alisema chama kushiriki uchaguzi ni jambo la hiyari na tume ya uchaguzi iko pale kwa ajili  ya kuweka na kutengeza mazingira yatakayofanya vyama vya siasa kushirki uchaguzi.

Alisema iwapo kuna chama kitaamua kutoshiriki uchaguzi, chama kitakachoshiriki hata kama ni mmoja mgombea wake atapita bila kupingwa.  Alisistiza kuwa hakuna sehemu yoyote ya katiba na sheria ya uchaguzi inayotamka kwamba chama kisiposhiriki uchaguzi basi uchaguzi unaahirishwa. 

“Ila ikitokea vyama vikasusa vyote kushiriki kwenye uchaguzi hapo ndipo unaweza kuahirishwa kwa kuwa hakutakuwa na mgombea,”alifafanua mkurugenzi wakati alipokuwa anazungumza na baadhi ya waandishi wa habari ambao walitaka kupata ufafanuzi wa tume kuhusu tamko lililotolewea na mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe.

Hivyo ameviasa vyama vya siasa vinavyotishia kutoshiriki kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika majimbo matatu na kata sita kufuata mifumo ya kisheria ya kushughulikia malalamiko ya uchaguzi.

Aliitaja mifumo hiyo kuwa ni kuwasilisha malalamiko kwenye kamati ya maadili wakati wa kampeni,  wakati wa kuanza kupiga kura wakala akiwa na malalamiko anajaza fomu namba 14 na fomu namba 16 wakati upigaji kura unapoeendelea  na kama mgombea hakuridhikai anaruhusiwa kwenda mahakamani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...