Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Edina Sanga (wa pili kushoto) akiwa na Afisa Polisi Kutoka dawati la Jinsia Christina Onyango na wadau mbalimbali wa masuala ya ukatili wa kijinsia.
 
Katika kusaidia kupinga ukatili wa kijinsia, kituo cha usuluhishi( Crisis Resolving Centre- CRC) kimejizatiti katika kutetea haki za binadamu kwa kulinda haki na ustawi wa watoto na wanawake.

Kituo hicho kilichoanzishwa 2007 kikiwa na mlengo wa utoaji huduma ya msaada wa kisheria  na ushauri nasaha kwa jamii.

Akizungumzia kazi zinazofanywa na CRC, Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi CRC Gladness Munuo amesema kuwa mnano Novemba 14 hafi 16 kimeweza kutoa ya huduma ya pamoja  kwa wahanga wa wa ukatili wa kijinsia  ijulikanayo kama One Stop Centre ikiwa inawalenga wakina mama na watoto ambao ndio waathirika wakubwa wa ukatili wa kijinsia.
Gladness amesema katika huduma ya pamoja na One Stop Centre  waliweza kutoa huduma kwa wateja 25 waliotembelea  kituo kwa kuhitaji msaada wakisheria na ushauri nasaha  ambapo wanawake walikuwa 22, wanaume 2 na mtoto mmoja.

Katika kesi hizo kesi mbili ziliweza kuhamishwa kutoka kituoni ambazo ni mgogoro wa ardhi na nyingine ilihusu kesi ya mauaji ambapo iliwezw kuhamishiwa polisi.

Ameelezea kuwa, katika usulihishi wa kifamilia uliweza kufanyika kwa wateja wanne na mashauri mawili ndio yaliyofanikiwa na nyingine ilikuwa ni matunzo ya mtoto.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...