Serikali imesema Wachimbaji wa Madini ya Jasi walioshindwa kuendeleza maeneo yao sheria itachukua mkondo wake ikiwemo kufutiwa leseni zao na maeneo yao kumilikishwa Wachimbaji wengine wenye nia ya kufanya uchimbaji.

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo alisema hayo Desemba 11, 2017 wakati wa ziara yake kwenye machimbo ya Jasi Wilayani Manyoni, Mkoani Singida.

Nyongo alitoa kauli hiyo kufuatia malalamiko ya baadhi ya wachimbaji wa madini hayo ya kukosa maeneo ya kutosha kufanya shughuli za uchimbaji husika na huku maeneo mengi yakiwa chini ya umiliki wa watu wasioyaendeleza.

Alisema leseni zilitolewa ili uchimbaji ufanyike na kwakua waliopewa leseni wameshindwa kuendeleza maeneo husika, sheria itachukua mkondo wake ikiwemo kuwaandikia hati ya makosa (default notice) na endapo watashindwa kutekeleza maelekezo watakayopewa, leseni za uchimbaji wa madini husika zitafutwa na maeneo yao kumilikishwa wengine.

Alimuagiza Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati, Singida, Sosthenes Massola kufuatilia suala hilo ili hatua stahiki zichukuliwe mapema iwezekanavyo. 

 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (aliyesimama) akizungumza na Wafanyakazi, Wachimbaji na Wafanyabiashara wa Madini ya Jasi (hawapo pichani) wakati wa ziara yake Itigi Mkoani Singida. Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Pius Luhende.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) akitembelea Kiwanda cha kuzalisha Chaki cha Dobercolor kilichopo katika Kijiji cha Majengo, Itigi. Kulia ni Mlinzi Mkuu wa Kiwanda hicho, John Kitika akielekeza eneo linalotumiwa kwa ajili ya kuanikia Chaki (halionekani pichani). Kuhoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Pius Luhende.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa tatu kushoto) akitazama mtambo wa kusaga Madini ya Jasi na kisha unga wake (gypsum powder) hutumika kutengeneza Chaki katika kiwanda cha Dobercolor kilichopo katika Kijiji cha Majengo, Itigi.

 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kushoto) akitazama hatua ya uchomaji wa Madini ya Jasi kwenye kiwanda cha kampuni ya mzawa cha RSR kinachomilikiwa na Rashid Rashid (kushoto) kilichopo katika Kijiji cha Sanjaranda, Itigi kabla ya kusagwa kuwa unga (Gypsum powder) na baadaye kusafirishwa hadi Dar es Salaam kwa ajili ya kuuzwa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...