Maofisa wa NBC wakiendesha
droo ya pili ya Kampeni ya Akaunti ya Malengo ya benki hiyo jijini Dar es
Salaam jana. Kutoka kushoto ni Humudi Semvua kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha,
Meneja Masoko wa NBC, Alina Kimaryo, Meneja
Amana za Wateja, Dorothea Mabonye na Meneja Maendeleo ya Biashara wa NBC, Amos
lyimo. Jumla ya washindi 12 wakijishindiaa kila mmoja shs milioni 1.
Meneja Masoko wa NBC, Alina
Kimaryo (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uchezeshaji wa
droo ya pili ya Kampeni ya Akaunti ya Malengo ya benki hiyo jijini Dar es
Salaam jana ambapo washindi 12 walijishindia kila mmoja shs milioni 1. Katikati
ni Meneja Amana za Wateja wa NBC, Dorothea Mabonye na Meneja Maendeleo ya
Biashara wa NBC, Amos Lyimo.
Meneja Maendeleo ya Biashara
wa NBC, Amos Lyimo (kulia) akipiga simu kwa mmoja wa washindi wakati wa droo ya pili ya Kampeni ya Akaunti
ya Malengo ya benki hiyo jijini Dar es Salaam jana. Wengine kutoka kushoto ni
Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Humudi Semvua, Meneja Masoko wa NBC,
Alina Kimaryo na Meneja wa Amana za Wateja, Dorothea Mabonye. Washindi 12
walijishindia shs milioni 1 kila mmoja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...