*Amshukuru Rais ,Dk. Magufuli kwa uamuzi wa kuanzisha wilaya hiyo

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando amesema kwa kushirikiana na wananchi wameendelea kutatua changamoto zilizopo wilayani humo huku akielezea hatua kwa hatua miradi mbalimbali ya kimaendeleo inayoendelea kufanywa.

ASHUKURU UAMUZI WA RAIS

Akizungumza kwenye mahojiano maalumu na Michuz Blogu, leo kwa njia ya simu , Mhando amesema wanamshukuru Rais ,Dk.John Magufuli kwa uamuzi wake wa kuanzisha Wilaya ya Tanganyika kwani imesaidia kusogeza mamlaka karibu, hali iliyochangia kutatuliwa kwa changamoto na kuboreshwa kwa miundombinu ya kimaendeleo.

"Tunamshukuru Rais uamuzi wake wa kuanzisha Wilaya ya Tanganyika iliyoanzishwa rasmi Julai Mosi mwaka 2016.Uwepo wa wilaya hii kumesaidia kwa sehemu kubwa kusogeza huduma kwa wananchi."Uwepo wa wilaya hii kumesaidia kuimarika kwa mindombonu hasa kwa kuzingatia ni wilaya ambayo ipo mpakani.Kwa sehemu kubwa tunampongeza Rais kwa uamuzi wake wa kuona haja ya kuwa na wilaya ya Tanganyika kwani inasukuma kwa kasi maendeleo ya wananchi,"amesema Mhando.

UMEME WILAYANI TANGANYIKA 

Kuhusu nishati ya umeme katika Wilaya hiyo, Mhando anasema kuwa kuna mikakati mingi inayoendelea ya kufanikisha nishati ya umeme inakuwepo katika maeneo yote na kufafanua tayari umeme umefika makao makuu ya wilaya."Wilaya ya Tanganyika ilianza kupata umeme mwaka 2017 baada ya kuanza kusambazwa kwa nguzo za umeme na sasa makao makuu ya wilaya tuna umeme, pia taasisi kadhaa pamoja na kaya 62 tayari nazo zimeanza kupata umeme.

"Malengo yetu ni kuendelea kuweka mikakati ambao utatusaidia kusogeza nishati ya umeme kwa wananchi wa Wilaya ya Tanganyika na hakika tunakwenda vizuri kwani Serikali Kuu nayo imekuwa ikituangalia kwa jicho la aina yeke."Imekuwa ikitoa fedha kwa ajili ya kuendelea na miradi ya kimaendeleo na hasa inayohusu kutatua changamoto zilizopo ikiwamo hii ya umeme,"amesema Mhando.

MIUNDOMBINU YA BARABARA

Akizungumzia miundombinu ya barabara, Mhando anasema Wilaya ya Tanganyika imeendelea kufunguka, kwani wanaendelea kuboresha barabara zilizopo ndani ya wilaya hiyo na zile ambazo zinatoka nje ya wilaya yao."Tunaendelea na ujenzi wa miundombinu ya barabara , kwa kueleza tu tayari barabara za Mpanda hadi Kalema na ile ya Mpanda Uvinza zimekamilika.Pia kuna mradi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 35 kutoka Vikonge hadi Mpanda.

"Tumedhamiria kuhakikisha tunakuwa na barabara za uhakika zitakazopitika wakati wa wote yaani masika na kiangazi na tumeanza kufanikiwa kwenye hili,"amesema Mhando.
MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando akishirikiana na Wananchi katika kazi ya ujenzi wa wilaya mpya ya Tanganyika ,mkoani Katavi ."Tumeanzisha ujenzi wa Sekondari ktk Kata 5 kati ya 8 ambazo hazina kabisa Sekondari za Kata,Lengo ni kuhakikisha ifikapo Disemba 2018 kata zote 8 zinakuwa na Sekondari"alisema DC Mhando
MKUU wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando akishirikiana na Wananchi katika kazi ya ujenzi wa wilaya mpya ya Tanganyika ,mkoani Katavi ."Tumeanzisha ujenzi wa Sekondari ktk Kata 5 kati ya 8 ambazo hazina kabisa Sekondari za Kata,Lengo ni kuhakikisha ifikapo Disemba 2018 kata zote 8 zinakuwa na Sekondari"alisema DC Mhando.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...