Na Hafidh Kido, Moshi.

KWA nafasi yangu ya msemaji wa timu ya Coastal Union 'Wagosi wa Kaya' ninatakiwa kusafiri na timu popote iendapo lakini kutokana na majukumu mengine nashindwa kutenda haya.

Lakini nilijiapiza mechi baina ya Wagosi na Polisi Tanzania iliyochezwa mjini Moshi katika uwanja wa Chuo cha Ushirika lazima niende. Kwa bahati ikatokea dharura ya kifamilia nikapata ruhusa kibaruani nami nikahudhuria.

Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwepo na maneno kuwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), anaikingia kifua Coastal Union kwa sababu ni mwenyeji wa Tanga lakini pia aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali za kiuongozi kwenye klabu hiyo kongwe ya jijini Tanga iliyoanzishwa mwaka 1948.

Kama hiyo haitoshi ikaelezwa kuwa kikosi cha Coastal Union kinacheza soka kwa kubebwa waamuzi ambao wanapokea maagizo kutoka TFF.

Yamezungumzwa mengi, itoshe tu kusema baadhi ya klabu zinazoshiriki Ligi ya soka Daraja la kwanza wamekuwa na malalamiko ya mara kwa mara kudai Coastal Union inabebwa.

Nimeamua kuja kushuhudia 'kubebwa' kwa Coastal Union. Naomba nitangaze maslahi kabla sijaendelea na andiko hili nililoliandika saa nane usiku wa kuamkia Jumapili Januari 21, 2018 nikiwa chumba cha hoteli Mjini Moshi Mkoa wa Kilimanjaro.

Mimi ni shabiki wa Coastal Union lakini pia ni mwanahabari. Hivyo naandika kwa jicho la kihabari lakini naweza kuteleza nikaweka unazi katika andiko hili. Nipo tayari kukosolewa na hata kuzodolewa ikiwa nitaandika uongo au kuongeza chumvi.

Hadi naandika haya msimamo wa kundi B inayojumuisha timu nane yaani Coastal Union, Polisi Tanzania, JKT Mlale, Kinondoni Manicipal (KMC), Mbeya Kwanza, Mufindi United, Mawenzi Market na Polisi Dar es Salaam.

Coastal Union ilikuwa inaongoza kundi kwa jumla ya alama 22, ikifuatiwa na Polisi Tanzania (21), JKT Mlale (21), KMC (19), Mbeya Kwanza (16), Mufindi Utd (12), Mawenzi Market (7) na Polisi DSM (3).

Kwa namna yoyote ile Polisi Tanzania wameumizwa na suluhu tuliyowalazimisha katika uwanja wao. Hivyo walijiandaa kwa hali yoyote iwayo kuhakikisha tunawaachia alama tatu muhimu kwao ili kujihakikishia kupanda Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...