Jalada la kesi ya  utakatishaji wa fedha inayomkabili aliyekuwa rais wa (TFF), Jamal Malinzi na wenzake limerudishwa Takukuru  kwa maagizo ya kurekebisha vitu vichache ili kukamilisha iuchunguzi.

Mbali ya Malinzi, wengine ni Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Msiande Mwanga. Wakili wa serikali kutoka Takukuru, Leornad Swai amedai hayo leo mbele ya Hakimu  Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, pindi shauri hilo lilipoitishwa kwa ajili ya kutajwa.

Swai alidai jalada la kesi hiyo limesharudishwa Takukuru likitokea kwa mkurugenzi wa mashtaka  DPP na kudai wamepewa maelekezo ya kukamilisha baadhi ya uchunguzi.Hata hivyo, wakili wa Utetezi Nehemia Nkonko aliomba upelelezi dhidi ya kesi hiyo ukamilike kwa haraka kwa sababu washtakiwa wapo ndani.

Hakimu Mashauri amahirisha kesi hiyo hadi January 25, 2018 kwa ajili ya kutajwa.Washtakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 28, yakiwemo ya kughushi na utakatishaji fedha ambazo ni Dola za Marekani, 375,418.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...