Imeandaliwa na ​ Geofrey Chambua ​kutoka vyanzo mbalimbali

Huenda umewahi kuliona na kulipita tu ama kutovutiwa na ladha yake ama kukereka na utomvu wake baada ya kula

Habari mbaya kwako ni kwamba umekosa kitu adimu na maridhawa sana......Hili ni moja ya matunda yanayochukuliwa kama MFALME WA MATUNDA (The King of Fruits) kwa kuwa na karibu vitamin vyote muhimu yaani A, B1, B2 na C..

Na sehemu zinazotumika ni majani, matunda, utomvu, mizizi na magamba. Na mfenesi unaweza kukua hadi kufikia kimo cha mita 20.........na nakusihi sana kuanzia leo ujitahidi kula walau punje tatu tu na ukiweza hata mbegu zake kwa kadri ya mada hii

Leo nimejikuta tu nafukunyua tunda hili baada ya kulikuta mahali fulani na jinsi watu walivyokuwa wanatua kilich cha thamani ndipo nilipoanza kugoogle nikakuta faida na hata hilo jina la lugha ya malkia huitwa Jackfruit

Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee huku likiwa na ladha tamu isiyomithilika. Licha ya sifa hii, tunda hili linatajwa kuwa na faida lukuki endapo litaliwa na mwanadamu.
Hakuna anayejua vizuri asili ya mafenesi lakini inaaminika asili yake ni katika misitu ya mvua nyingi ya Magharibi ya ghats (western ghats). Lakini kwa sasa inalimwa katika nchi za india, Burma, Sri lanka, China, Malaya, East in indies, Qeens land, Maturities, Hawaii, Suriname, Brazil, Kenya, Uganda na Tanzania, Na nchini Tanzania hulimwa Pemba, Unguja, Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Tanga na Mbeya(Kyela) nk.

Kwanza, linatajwa kuwa na virutubisho kadha wa kadha vyenye kazi mbalimbali mwilini. Baadhi ya virutubisho hivyo ni pamoja na vitamini za aina mbalimbali, madini, protini, mafuta, uwanga na nyuzinyuz (fiber) ambazo husaidia kwenye mfumo wa mmeng'enyo na kuchagiza tatizo la kupata haja (constipation) na linasaidia pia kuzuiwa kuvimbiwa.

Fenesi pia linatajwa kuwa chanzo kizuri cha nishati kisichokuwa na lehemu (cholesterol). Si hivyo tu, bali pia ni chakula chenye virutubisho vya kuondosha sumu mwilini vinavyoweza kuukinga mwili dhidi ya saratani na magonjwa mengine kadha wa kadha,

Sukari ya Fenesi ni dawa ya sukari sumu mwilini kwa kuwa linasharabiwa taratibu mwilini na kufyonza sukari sumu na hii husaidia pia katika kuhibiti shinikizo la damu mwilini ( Jackfruit is more slowly absorbed into the bloodstream, which prevents sugar crashes, sugar cravings, and mood swings, They are well known because of its high potassium content. This helps the blood vessels relax and maintains proper blood pressure.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...