Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiteta jambo Ofisini kwake  na Maafisa Watendaji wa Asasi ya International Youth Fellowship(IYF), leo Januari 23, 2018 walipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza ambapo Watendaji wa Asasi hiyo wamewalisha mada kuhusu mafunzo yanayolenga mabadiliko ya mitizamo kwa wafungwa katika kuachana na tabia za kihalifu mara wamalizapo vifungo magerezani.  
 Mkurugenzi Mkazi wa Asasi ya International Youth Fellowship (IYF),  Jeon Hee yong akitoa mada mbele ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) kuhusiana na mabadiliko ya mitizamo kwa wafungwa katika kuachana na tabia za kihalifu mara wamalizapo vifungo vyao magerezani
 Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa umakini mada kutoka kwa Watendaji wa Asasi ya International Youth Fellowship (IYF) katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza(wa kwanza kushoto) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila..
  Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akitoa taarifa fupi kabla ya  Watendaji wa Asasi ya International Youth Fellowship (IYFkuwasilisha mada yao katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza leo Januari 23, 2018.
 Kikundi cha Kwaya cha Asasi ya International Youth Fellowship ambacho kinaundwa raia kutoka nchini Korea kikitumbuiza kabla ya uwasilishaji wa mada kama inavyoonekana katika picha.
 Wataalam wa Jeshi la Magereza wakifuatilia Mada kuhusu mabadiliko ya mitizamo kwa wafungwa katika kuachana na tabia za kihalifu.
Kamishna Jenaerali wa Magereza Nchini, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Asasi ya International Youth Fellowship walioketi(wa kwanza kushoto) ni  Mkurugenzi Mkazi wa Asasi hiyo Bw. Jeon Hee yong(wa kwanza kulia) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila. Wengine waliosimama mstari wa nyuma ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza, leo Januari 23, 2018 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...