Mkoa wa Mtwara Umeanza Kufanya Uhamasishaji wa Kuondoa Mimba za Utotoni na Wanafunzi wanaoacha Shule kutokana na Sababu Mbalimbali zinazowakumba Wanafunzi wa Kike kwa Njia ya Sanaa ya Maigizo.

Kupitia kituo cha Sports Development Aid (SDA) tayari kimefanya Mafunzo ya Sanaa ya Maigizo kwa Kuwatumia Waigizaji wenye Mafanikio kwa lengo la kutoa elimu kwa Wanafunzi wa Jinsia zote katika Shule ya Sekondari ya Shangani.

Kituo cha SDA tayari kimeanza Kutoa Mafunzo ya Elimu ya Jinsia kwa shule za Mtwara mjini na Vijijini kwa Kutumia njia ya Michezo, ambapo imekuwa ikigawa Vifaa vya Michezo pamoja na Kukarabati Viwanja Michezo vya Shule.
 Msanii wa Maigizo Yvone Sherry (Monalisa)Akiongea na Wanafunzi wa Shangani Sekondari mkoani Mtwara pamoja kusimamia Igizo La Elim ya Jinsia kwa njia ya Maigizo.
 Viongozi wa Kituo cha Sports Development Aid (SDA) ambao ndio waandaaji wa Mafunzo hayo wakiongea na Wanafunzi wa Sekondari ya Shangani Iliyopo mkoani Mtwara.
 Pichani ni Afisa taalum wa Mkoa wa Mtwara Masalanga akiongea na Wanafunzi wa Sekondari ya Shangani katika Mafunzo kupitia Sanaa ya Maigizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...