Sisi, Familia ya Mrs Bdariya Ramadhan Kiondo (Aliekuwa Afisa waMambo ya Nje Mkuu na Mkuu wa Utawala na Fedha katika Ubalozi wa Tanzania New Delhi, India, tunamshukuru Mungu kwa zawadi aliotupa kwetu kama Mke,Mama,Bibi, Shangazi ,Ndugu na kwa mwili wa kumcha Mungu.
Tunashukuru kwa upendo mkuu,kwa kushiriki nasi katika kumsindikiza mpendwa wetu katika nyumba yake ya milele tarehe 15 Desemba  2017.Tunapenda kuwashukuru marafiki,ndugu, Wafanyakazi wa Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Watumishi wenzake katika Ubalozi wa Tanzania Nchini New Delhi,India, marafiki na Ndugu wote kutoka Nchi mbali  mbali Duniani,(hasa India,,Uingereza, Uholanzi, Canada, Oman UAE na USA).
Shukran za pekee pia ziwafikie Madaktari wake wote katika Hospitali ya Apollo New Delhi,Mwambata Tiba katika Ubalozi wetu New Delhi kwa juhudi kubwa waliofanya katika matibabu yake, Viongozi Wakuu mbali mbali Serikalini,Balozi na Wafanyakazi wa Ubalozi wetu New Delhi India,Uongozi na wafanyakazi wa Wizara ya mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika mashariki,Majirani wa Kiondoni Ada Estate flats, ndugu na jamaa wote kutoka Zanzibar,Tanga na Msikiti wa Al Maamur ,Upanga Dar es salaam. Asanteni Sana.
Kisomo cha 40 ya Marehemu kitakuwa  tarehe 27 January 2018 huko Mkwajuni, Kivunge Kijijini, kwa Foum Kimara, Zanzibar baada ya Swala ya Adhuhuri (Saa saba mchana). Wote mnakaribishwa kushiriki nasi.
Ni vigumu kumshukuru kila mmoja kwa majina tunaomba mlioshiriki kwa namna moja au nyingine mpokee shukrani  zetu hizi za upendo kwa kuwa nasi katika kipindi hiki kigumu.
Tunaendelea kuomba Roho ya mpendwa wetu “B”ipumzike kwa Amani na utakuwa nasi daima milele Amen.

Pumzika kwa Amanai Mpendwa wetu.                                    
Innalilah wainailah rajiun.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...