Na Agness Francis, Globu ya Jamii

KAMPUNI ya simu za mkononi Airtel imetangaza rasmi kugawa gawio la Sh.bilioni 1.7 kwa kila robo ya mwaka kwa wateja wake wote wanaotumia Airtel Money  ikiwa ni mara ya tano kufanyika tangu ianzishwe huduma hiyo mwaka 2015.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Masomo Airtel  Money Isack Nchunda, amesema kuwa leo wametoa rasmi Sh, bilioni 1.7 ambayo ni riba ya robo ya mwaka iliyopita  ikiwa zoezi hilo litakuwa endelevu badala ya ule utaratibu wa mwanzowa kila  miezi sita ambapo gawio hilo la faida litawafikia moja kwa moja  walengwa ambao ni wateja pamoja na mawakala wote wanaotumia huduma hiyo ya Airtel Money hapa nchini. 

Amefafanua Nchunda amesema Mr. Money atarudisha gawio kulingana na salio linalosalia katika akaunti kila siku kwa anayetumia huduma hiyo ambayo mteja atakuwa huru kufanya matumizi yake binafsi kama kununua bando, luku, na mahitaji mengine kupitia riba hiyo bila kupangiwa na Mr. Money  huyo.

Kwa upande wake Meneja wa Huduma za Airtel Money Ibrahim Malando, amewataka mawakala hao kuendelea kufanya huduma bora kwa wateja wao kwani ni hatua nzuri ya kujiongezea zaidi faida kwa gawio lijalo.
Mkurugenzi wa masomo Airtel Tanzania Isack Nchunda akiongea Jijini Dar es Salaam leo wakati wa gawio kwa wateja na mawakala wa Airtel money ambapo jumla Sh bilioni 1.7 zitatolewa kwa robo ya mwaka iliyoisha Disemba 2017.kushoto ni Meneja huduma za Airtel money  Ibrahim Malando na Meneja uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando.

 Meneja huduma za Airtel money Ibrahim Malando akiongea Jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutangaza gawio kwa wateja na mawakala wa Airtel money ambapo jumla y sh bilioni 1.7 zitatilewa kwa robo ya mwaka iliyoisha Disemba 2017 katika ni Mkurugenzi wa masoko Airtel money Tanzania Isack Nchunda  na Meneja  uhusiano wa Airtel  Tanzania Jackson  Mmbando

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...