Na Agness Francis-Globu ya jamii

TIMU Soka ya Yanga inatarajia kushuka dimbani kesho kuvaana na timu ya Mwadui Fc katika mchezo wa raundi ya 13 ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Vodavom Tanzania Bara. 

Mchezo huo utachezwa saa 10 jioni Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam maarufu la Shamba la Bibi.Katika mechi ya raundi ya 12 Yanga walipoteza mchezo wao dhidi ya Mbao FC uliochezwa jijini Mwanza katika Uwanja wa CCM Kirumba 

Mabingwa hao watetezi watashuka dimbani huku wakimkosa mshambuliaji wake wa kimataifa kutoka nchini Zambia Obrey Chirwa aliyefungiwa mechi tatu na Kamati ya Nidhamu ya TFF. Pia watamkosa mshambuliaji wao kutoka Zimbabwe Donard Ngoma ambaye bado hajawa fiti. 

Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga Boniphace Mkwasa amesema maandalizi ni mazuri na wanajua mchezo huo utakuwa mgumu.

“Tumejipanga kupambana kuhakikisha tunashinda mchezo wetu wa kesho,” amesisitiza Mkwasa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...