Na Agness Francis, Blogu ya jamii 
KLABU ya Yanga ya Dar es Salaam imesaini mkataba wa miaka mitatu na Kampuni ya Macron kutoka  Itali kwa lengo la kutengenezewa jezi za kimataifa zenye thamani ya Sh.bilioni 2.

Makubaliano ya utiaji saini mkataba huo umefanywa leo Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Yanga Boniphace Mkwasa na Mkurugenzi Kampuni ya Macron Tanzania Suleiman Karimu.

Akizungumza baada kusaini mkataba huo, Mkwasa pia amesema kwa wale wanaouza jezi mitaani kwa manufaa yao binafsi ambayo  hayanufaishi klabu yao waache mara moja.

"Kwa wataoendelea na biashara hiyo watachukuliwa hatua,"amesema Mkwasa.

Kwa upande wa Mkurugenzi kampuni ya Macron Tanzania, Suleiman Karimu ameishukuru klabu ya Yanga kwani  makubaliano hayo  yataleta mapinduzi ya mpira wa miguu hapa nchini.
Katibu Mkuu wa Yanga Charles Mkwasa akisaini makubaliano ya mkataba na Mkurugenzi wa MACRON Tanzania Suleiman Karim wenye thamani ya Bilion 2 kwa ajili ya vifaa vya michezo uliotiwa saini leo Mbele ya waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...