Zoezi la ugawaji wa Miguu ya kisasa ya bandia kwa watu wenye ulemavu wa Miguu awamu ya pili limeanza jana, ikiwa ni Kampeni iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ya kuwapatia Miguu ya kisasa inayowawezesha kufanya shughuli za uzalishaji Mali Kama awali ambapo imejidhihirisha kuwa RC Makonda akiahidi jambo analitimiza kwa vitendo na sio Siasa.

Katika awamu ya pili iliyoanza jana zaidi ya Walemavu 108 wamepatiwa Miguu ya kisasa ya Bandia ambayo inakadiriwa Mguu mmoja unagharimu kiasi cha shilling million 2 hadi 3 ambapo yote kwa pamoja ni Shilling Million 324,000,000 lakini kwa jitiada za RC Makonda wamepatiwa Miguu hiyo Bure.

Katika awamu ya Kwanza jumla ya Wagonjwa 35 wa kisukari walipatiwa miguu ya kisasa ya bandia yenye thamani ya Shilling million 157 kutoka CCBRT na kufanya jumla ya walemavu waliopatiwa miguu hiyo kufikia 143 yenye thamani ya Million 481 Bure.

Baadhi ya Walemavu waliopatiwa Miguu hiyo wamemshukuru RC Makonda kwa moyo wa pekee wa kuwajali wananchi wake kwa kuzingatia makundi yote kwenye jamii ambapo wamesema kwa sasa wataenda kufanya kazi na kuachana na utegemezi.

Aidha wameishukuru kampuni ya Kamal Group kwa kumuunga mkono RC Makonda kutimiza maono yake ya kuwawezesha walemavu kupata miguu ya kisasa inayowawezesha kufanya shughuli za kujiingizia kipato.
  Baadhi ya Walemavu 108 wamepatiwa Miguu ya kisasa ya Bandia ambayo inakadiriwa kuwa Mguu mmoja unagharimu kiasi cha shilling million 2 hadi 3 ambapo yote kwa pamoja ni Shilling Million 324,000,000 lakini kwa jitihada za RC Makonda wamepatiwa Miguu hiyo Bure.
 Iliuwa ni furaha kwa Walemavu hao kupatiwa miguu ya bandia bure
  Miguu ya kisasa ya Bandia ikiwa tayari kugaiwa kwa walengwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...