Na Agness Francis Globu ya jamii 
Mabingwa Afrika Mashariki na kati AzamFc watashuka dimbani kufuana na  timu ya  KMC FC  katika kuwania Kombe ya FA hukuwa wakiwa wenyeji wa kikosi hicho. 

AzamFC watakuwa wageni dhidi ya timu hiyo katika Uwanja wa Azam Complex ambapo KMC watautumia uwanja huo kama wa nyumbani, ikiwa mchezo huo utapigwa saa moja jioni. 

Akizungumza Ofisa Habari wa AzamFc Jaffary Iddy Maganga katika ofisi zao Mzizi Jijini Dar es Salaam, amesema kuwa timu imesharejea nyumbani kutokea Mkoani Iringa ambapo walikuwa na mchezo wao dhidi ya Lipuli waliotoka sare bila kufungana. 

Aidha amesema kikosi kimeshaingia kambini na kimeshaanza mazoezi  katika kuelekea mtanange huo dhidi ya KMC. 

"Mchezo ni mgumu unajitahid juhudi za hali ya juu ukizingatia  kikosi hicho ni kizuri na itakuwa lazima mmoja atoke ili kuelekea Mchuano wa Robo Fainali kombe la FA," amesema Maganga.

Hata hivyo,wachezaji wa AzamFC walikuwa majeruhi karibuni wote wako fiti isipokuwa Kiungo mkabaji Himidi Mau Mkami. 

"Tutaendelea kumkosa Himid Mau takribani kwa wiki 3 kwa sasa yupo nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ambapo Daktari amesema kuwa ana uvimbe uliovilia damu kwenye goti lake,"amesema Jaffary Maganga.
Afisa Habari wa AzamFc Jaffary Iddy Maganga, akizungumza na waandishi wa habari  leo katika Ofisi zao Jijini Dar es Salaam kuhusu mchezo wao dhidi ya KMC utaorindima pale Azam Complex Chamazi siku ya Jumamosi tarehe 24 majira ya sa 1 Usiku ambapo watakuwa wageni wa mchezo huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...