Na Said Mwishehe, Globu ya jamii.
BENKI ya Equity imezindua huduma za kibenki kwa njia ya mtandao  ambapo wateja wao sasa watapata huduma mahali popote kupitia  simu za mkononi, tablets na kompyuta za mezani na mpakato.

Huduma hizo watazipata kupitia Eazzy Banking kwa kufanya miamala  kirahisi iwe usiku au mchana, wakiwa nyumbani, au ofisini na kubwa zaidi sasa watakuwa na nafasi ya kuokoa muda na gharama.

Akizungumza Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Eazzy Banking,  Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Joseph Iha amesema kuwa huduma  hizo mpya zitatoa fursa kwa wateja kufanya miala mahali popote.

"Huduma za Eazzy Banking zitaambana na EazzyBanking App, app ya  kimataifa ya masuala ya kifedha inayounganisha huduma za laini za simu na kuwawezesha wateja kutuma fedha na pia kufanya malipo kupitia simu zao popote walipo na wakati wowote.

"EazzyBanking ni rahisi kuianzisha na hutoa huduma za kipekee kama  kutuma fedha kwenda akaunti za benki au mitandao ya simu, kuomba na kulipia mikopo , kulipia bili(ankara) na aina ya huduma za malipo," amesema Iha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Equity, Joseph Iha akizungumza na wageni waalikwa na wanahabari waliofika katika uzinduzi uliofanyika jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa huduma ya Eazzy Banking inayomsaidia mteja kufanya miamala yake bila stress wakati wowote 24/7 popote atakapokuwa.
Wateja walihudhuria uzinduzi wa huduma ya Eazzy Banking inayotolewa na benki ya Equity jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Equity Joseph Iha akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam kutoa ufafanuzi wa masuala mbali mbali mara baada ya uzinduzi wa huduma ya Eazzy Banking inayomsaidia mteja kufanya miamala yake bila stress wakati wowote 24/7 popote atakapokuwa. Pembeni ni wakurugenzi wa Bodi ya Benki hiyo ikiongozwa na Simbeye.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...