Uwekezaji katika sekta ya elimu Nchini kupitia mpango wa kuinua ubora wa elimu (EQUIP-Tanzania) ambao umelenga kuboresha mchakato wa kufundisha na matokeo ya kujifunza kwa watoto nchini umeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa Mkoani Simiyu.

Uwekezaji huo ambao unafadhiliwa na serikali ya Uingereza kupitia Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) umeleta ufanisi wa elimu na kufanya viwango cha ufaulu kuwa juu kutoka asilimia 36 mwaka 2013 mpaka asilimia 68 2017.

Na katika kutimiza hayo Jumla ya kiasi cha shilingi Bil 1.7 kutoka DFID kupitia mradi wa kuinua ubora wa Elimu Nchini (Equip) zimetolewa kwa Serikali ya Mkoani Simiyu kwa ajili ya kujenga na kuboresha miundombinu ya elimu Mkoani humo .

Akizungumzia nia ya serikali ya Uingereza wakati wa mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan , Mkuu wa DFID-Tanzania Elizabeth Arthy alisema wametoa kiasi hicho cha fedha kwa serikali ya Mkoa wa Simiyu ili kuhakikisha wanatatua changamoto ya miundombinu iliyopo.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mheshimiwa Anthony Mtaka akimuelezea Makamu wa Raisi utekelezaji wa mpango wa EQUIP-Tanzania mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza nchini Tanzania Bibi Elizabeth Arthy akizungumza mbele ya makamu wa Rais juu ya mchango wa serikali ya Uingereza katika kuboresha elimu.
Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza nchini Tanzania Bibi Elizabeth Arthy akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa shule ya msingi Gamondo A iliyoo wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...