Chama cha Urafiki wa Wananchi wa Nchi ya Tanzania Na Msumbiji TAMOFA Kimempa Ubalozi Bondia wa Kimataifa Francis Cheka Ili kuweza Kutangaza Chama Hicho kwa lengo la Kujipatia wafadhili ndani na nje ya nchi.

Akiongea mara baada ya makabidhiano ya kadi ya ubalozi Mkoani Mtwara Francis Cheka anasema Urafiki wa msumbiji na Tanzania Umekuwa wa Muda Mrefu na hivyo kuhamasisha wananchii kujiunga na chama hicho hasa wale wanaofanya safari katika nchi hizo mbili.

Hamza Lichete ni katibu mwenezi wa TAMOFA anasema kazi kubwa ya chama hicho ni kuimarisha Mahusiano pamoja na kulinda  Umoja  kati ya nchi hizi mbili kwa lengo la kuimarisha uchumi pamoja na amani.

Cheka ambaye kwa sasa anaishi Mkoani Mtwara amezaliwa Nchini Msumbiji lakini kwa kiasi kikubwa amekuwa akiitangaza Tanzania katika mapambano mbalimbali ya Kimataifa ambayo yamempatia umaarufu yeye pamoja  Na Nchi ya Tanzania

Chama cha TAMOFA kiliasisiwa na marasi Hayati Jullius Kambarage Nyerere pamoja na Samora Mashel mwaka 1987.
Bondia Francis Cheka akiwa amesimama Mbele ya Jengo la Ofisi ya TAMOFA maara baada ya Kupewa Ubalozi wa Chama Hicho Mkoani Mtwara.
 Bondia Francis Cheka akionesha Kadi ya Ubalozi wa TAMOFA kwa Waandishi wa Habari Mara Baada ya Kukabidhiwa Mkoani Mtwara.
Picha1.Mwenyekiti wa TAMOFA Kanda ya Kusini Seleman Mstapha Akimkabidhi Kadi ya Ubalozi wa TAMOFS bondia Francis Cheka Mkoani Mtwara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...