Meneja Masoko wa GSM Farida  Rubanza akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mshindi wa shidano la Disney ,Consolata Mlebusi mkazi wa Mbezi Beach  ambapo ataenda mapumziko.
Mwakilishi wa wateja aliyezungusha gurudumu hilo na kuokota ticket ya mshindi Edward Laurent Kapwapwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupatika mshindi wa shindano hilo.

Mshindi wa shidano la Disney lililokuwa linaendeshwa na kampuni ya Maduka ya GSM leo limefikia mwisho baada ya leo kuchezeshwa droo na kupata mshindi ambaye ataenda mapumziko huko Hong Kong.

Akizungumza wakati wa uchezeshaji shidano hilo Meneja Masoko wa GSM Farida  Rubanza amemtangaza mshindi wa shidano hilo kwa ni Consolata Mlebusi mkazi wa Mbezi Beach , mshindi huyo  amepatikana baada ya ticket yake kuokotwa baada ya kuzungushwa kwa gurudumu lenye Mamia ya ticket.

Aidha amewataka wateja wa maduka ya GSM kuendelea kutumia huduma zao kwa kuwa zina ubora .
Kwaupande wake  Mwakilishi wa wateja aliyezungusha gurudumu hilo na kuokota ticket ya mshindi Edward Laurent Kapwapwa, ameishukuru kampuni ya GSM kwa kuendesha shindano hilo kwa uwazi.

"Mimi nimekuja kununua vitu hapa dukani nimetoka Mtwara nimekuja hapa Dar es Salaam kwa kazi zangu nimeitwa tu na wameniomba  niokote ticket, kwanza huyu mshindi hata simfahamu, kwakweli nimeona shindano hili ni la haki na kweli  nawaomba watu wote na wateja wa GSM  kuendelea  kutumia bidhaa zao hata mimi hapa nimekuja kununua bidhaa zao" Alisema

Mshindi huyo atawasili muda wowote kufahamishwa taratibu za safari yake  amabapo kwa mujibu GSG anatakiwa kusafiri yeye na familia yake jumla wawe wanne, shindano hilo limedumu kwa muda wa miezi miwili Lilianza December 2017 hadi February 4,na leo kuchezeshwa droo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...