Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Mkazi Angelina Mabula amesema ni marufuku halmashauri kuchukua maeneo ya wananchi bila ya kuwalipa fidia.

Mhe. Mabula amesema hayo Wilayani Butiama mkoa Mara wakati wa ziara yake yenye nia ya kutatua migogoro ya ardhi pamoja na kukagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi.

Amesema wakati wa mchakato wa kuchukua maeneo ya mwananchi ni vyema wahusika wakashirikishwa kuanzia hatua ya awali sambambana na kuelimishwa juu ya zoezi hilo ili kuepuka migogoro inayoweza kutokea.

‘’cha msingi ni kuanza kuzungumza na mwananchi kabla ya kuchukua eneo lake na kumueleza eneo ambalo ataachiwa na halmashauri zihakikishe mwananchi huyo anapimiwa pamoja na kupatiwa hati yake’’ alisema Mabula

Aidha, mhe. Mabula amesema eneo litakalochukuliwa na halmashauri viwanja vyake kuuzwa fedha itakayopatikana halmashauri ihakikishe inatumika katika kutengeneza miundo mbinu na huduma nyingine za jamii na kusisitiza kuwa kwa kufanya hivyo migogoro haiwezi kutokea.

Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi ameziagiza halmashauri kuhakikisha zinapanga miji kulingana na ‘master plan’ ili kuwa miji bora iliyopangika.
Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Angelina mabula akizungumza na watumishi wa halmashauri za Mji na Wilaya ya musoma mkoa wa Mara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...