MJUMBE wa halmashauri kuu ya CCM Taifa anayewakilisha Mkoa wa Iringa Salim Asas ameichangia jumuiya ya wanawake wa chama cha mapinduzi ( UWT) wilaya ya Kilolo shilingi milioni 5 kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi wa kisasa wa mikutano.
Akifungua kikao cha baraza kuu la UWT Wilaya ya kilolo, Asas alisema kuwa lengo la kusaidia jumuiya hiyo ni kuitaka ijitegemee pia kuwa na miradi yake kwani ameona ni vema kuiwezesha jumuiya hiyo kupata ndoano kuliko kuipa samaki na kuwa kwa kipindi chake chote cha miaka mitano atakayokuwepo madarakani ataichangia jumuiya hiyo kiasi cha shilingi milioni 5 kwa ajili ya ujenzi huo "Ahadi yangu nitapaswa kuiweka katika maandishi ili familia yangu ijue pale nitakapo tangulia mbele za Haki ahadi hii iweze kutekelezwa na familia maana hatujui la kesho"
Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...