JESHI
la Polisi mkoani Mwanza kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) mkoani hapa imemkamata
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Bw. Anthony Bahebe.
Pia Mwanasheria wa Halmashauri hiyo Bw. Alphonce Sebukoto naye amekamatwa na Jeshi hilo.
Viongozi wote hao wanakabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na ubadhilifu wa fedha za umma.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, Ahmed
Msangi alisema kukamatwa kwa viongozi hao kunatokana na tuhuma
mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya
madaraka.
Kamanda
Msangi alisema, Bw. Sebukoto alikamatwa Februari 19, 2017 na Bw. Bahebe
amekamatwa leo na wote wanaendelea kuhojiwa na Polisi kwa kushirikiana
na TAKUKURU.
Naye Kamanda wa TAKUKURU wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Ernest Makale alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo ya sh.milioni 278 zilipwe katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. Bahebe.
Alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo hayo kwa Bw. Bahebe Novemba 2017 wakati alipokuwa anakaimu nafasi ya ukurugenzi wa Halmashauri ya Misungwi ambapo jumla sh. milioni 138 ziliingizwa katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti huyo.
Naye Kamanda wa TAKUKURU wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Ernest Makale alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo ya sh.milioni 278 zilipwe katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. Bahebe.
Alisema Bw. Sebukoto aliidhinisha malipo hayo kwa Bw. Bahebe Novemba 2017 wakati alipokuwa anakaimu nafasi ya ukurugenzi wa Halmashauri ya Misungwi ambapo jumla sh. milioni 138 ziliingizwa katika akaunti binafsi ya Mwenyekiti huyo.
Alisema kiasi kingine cha fedha kinachunguzwa kubaini kilipo.
Kukamatwa kwa viongozi hao kunatokana na juhudi za Serikali katika mapambado dhidi ya matumizi mabaya ya madaraka pamoja na fedha za umma.
Kukamatwa kwa viongozi hao kunatokana na juhudi za Serikali katika mapambado dhidi ya matumizi mabaya ya madaraka pamoja na fedha za umma.
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi, Anthony Bahebe akiwa chini ya
ulinzi baada ya kukamatwa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Taasisi
ya Kuzuia na Kuapamba na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) jijini Mwanza
Februari 21, 2018 kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na
ubadhilifu wa fedha za umma. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...