Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) unakusudia kuishawishi serikali na waajiri katika sekta binafsi hapa nchini kuitambua kada ya Usalama na Afya mahali pa kazi na kuiweka katika mfumo rasmi wa ajira.

Mpango huo uliwekwa wazi na Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi.Khadija Mwenda, alipowahutubia wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi katika hafla ya kufunga kozi hiyo Februari 23,2018 jijini Dar es salaam. Kozi hiyo pamoja na nyingine zinazohusu Usalama na Afya kazini hutolewa na Wakala huo wa serikali.

Mtendaji Mkuu huyo alisema kwasasa kada ya maofisa Usalama Mahali pa Kazi (Safety Officers) bado haitambuliki katika mfumo rasmi wa ajira hapa nchini jambo linalopunguza ufanisi katika kusimamia utekelezaji wa Sheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003.

”Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003, inawataka waajiri kuunda Kamati za Usalama na Afya katika sehemu zao za kazi ambazo wajumbe wake ni wawakilishi wa wafanyakazi ambao kimsingi wana majukumu yao mengine tofauti na kusimamia masuala ya usalama na afya mahali pa kazi. Hivyo jukumu la kusimamia usalama na afya wa wafanyakazi wenzao katika sehemu za kazi husika linakuwa ni la ziada,” alisema Bi. Mwenda.

Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akiwahutubia wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mafunzo, Utafiti na Takwimu wa OSHA, Bw. Joshua Matiko, akiongea na wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam.
Wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakifuatilia hotuba ya Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, wakati wa hafla ya kufunga kozi hiyo iliyofanyika katika ofisi za Wakala jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...