Na John Nditi, Globu ya Jamii Morogoro
MKUU wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe ameunda timu maalumu inayojumuisha  vyombo vya ulinzi na usalama itakayoshirikiana na wataalamu wa uthamini  wa Serikali na wenyeviti wa vitongoji vya vijiji vya Bwila Chini na Kiburumo , kata ya Selembala , halmashauri ya wilaya ya Morogoro   ili kuhakiki  upya majina  ya  waliolipwa  fedha za fidia na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) kwa ajili ya  kupisha ujenzi wa mradi  wa  bawawa la Kidunda .
Mkuu wa mkoa amelazimika kuunda timu hiyo baada ya kusikiliza malalamiko ya wananchi wa vijiji hivyo   wakati wa mkutano  wa  hadhara uliofanyika katika kijiji cha Bwila Chini  na kuhudhiriwa na mamia ya wananchi wa vijiji hivyo.
Dk Kebwe alisema  , ameiunda timu hiyo  licha ya pande zote kueleza kwa udani namna zoezi la uhakiki na uthamini wa  makazi ya watu wa vitongoji vinane  vya vijiji hivyo  kuelezwa kuwa zoezi hili lilifanyika  kwa uwazi ulioshirikisha  wenyeviti wao wa vitongoji na malipo kufanyika baada ya taratibu zote za kisheria kufuatwa.
Kwa nyakati  tofauti  baadhi ya wananchi waliopewa furasa ya kuuliza maswali wakidai kuwa wapo baadhi ya watu wamelipwa fedha za fidia  wakati zi  wakazi wa vitongoji vya vijiji hivyo  wakiwa hawana nyumba wala mashamba .
“ Nimelazimika niunde  timu  ya baadhi ya wajumbe wa kamati za ulinzi na usalama  itakayoshirikiana na wataalam na viongozi wa serikali za vitongoji kuhakiki majina yote kwa ajili ya kujiridhisha  ili kubaini  endapo madai  ya  wananchi  yanaukweli ama laa   na yakiwa na  ukweli hatua za kisheria zitachukuliwa  kwa wahusika” alisema Dk Kebwe.
 Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe ( kushoto)  akifungua kikao cha kusikiliza kero za  wananchi  wa vijiji vya Bwila Chini na Kiburumo , kata ya Selembala , halmashauri ya wilaya ya Morogoro  wakati wakiwasilisha changamoto mbalimbali  zikiwemo za malipo ya   fedha za fidia  kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA)  kwa ajili ya kupisha ujenzi wa mradi  wa  bawawa la Kidunda
 Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe ( kushoto)  akiwasiliza kero za  wananchi  wa vijiji vya Bwila Chini na Kiburumo , kata ya Selembala , halmashauri ya wilaya ya Morogoro  wakati wakiwasiisha changamoto mbalimbali  zikiwemo za malipo ya   fedha za fidia  kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA)  kwa ajili ya kupisha ujenzi wa mradi  wa  bawawa la Kidunda

 Sehemu ya wananchi  wa vijiji vya Bwila Chini na Kiburumo , kata ya Selembala , halmashauri ya wilaya ya Morogoro  wakimsikiliza mkuu mkoa  huo Dk Kebwe Stephen Kebwe ( hayupo pichani)  wakati akitoa majawabu ya changamoto mbalimbali  zikiwemo za malipo ya  fedha za fidia  kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA)  kwa ajili ya kupisha ujenzi wa mradi  wa  bawawa la Kidunda 
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Morogoro, Kibena Kingo ( aliyesimama meza kuu) akitoa maenezo ya ufafanuzi  mbele ya mkuu  wa mkoa  huo Dk Kebwe Stephen Kebwe  ( hauonekani pichani) kabla ya kusikiliza changamoto za   wananchi  wa vijiji vya Bwila Chini na Kiburumo , kata ya Selembala , iliyopo kwenye halmashauri hiyo.
Mkazi wa kijiji cha  Bwila Chini kata ya Selembala halmashauri ya wilaya ya Morogoro akitoa kero yake kwa mkuu mkoa  wa Morogoro Dk Kebwe Stephen Kebwe ( hayupo pichani)   wakati wa mkutano wake wa kusikilkiza changamoto mbalimbali  za wananchi wa vijiji viwili cha Bwila Chini na Kiburumo ambao wamelipwa   fedha za fidia  kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA)  ili  kupisha ujenzi wa mradi  wa bawawa la Kidunda. Picha na John Nditi. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...