Na Agness Francis Globu ya jamii. 

 VINARA wa Ligi kuu Tanzania Bara Simba SC mara baada ya kurejea kutoka nchini Djibout katika mchezo wa marudiano na Gendarmarie sasa wanaanza mazoezi rasmi leo ili kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Mbao FC. Mazoezi hayo yataanza leo jioni saa 10 jioni katika uwanja wa Boko Veterani jijini Dar es Salaam. 

 Ikiwa ni mzunguko wa 2 round ya 19 katika michuano ya kuania Ubingwa wa Tanzania Bara ambapo mchezo uliopita Simba alitoka sare ya 2-2 dhidi ya Mwadui FC katika Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga. 

 Hata hivyo Kikosi hicho kilipewa muda wa mapumziko ya siku moja baada ya kurejea kutoka nchini Djibout katika mchezo wa marudiano dhidi ya Gendarmerie ambapo kikosi cha Simba kiliibuka na Ushindi wa goli 1-0 na kujiandikishia tiketi ya kwenda hatua ya mbele zaidi katika Michuano ya kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...