Taxify, ambayo imejitanua katika utoaji wa huduma zake barani Ulaya na Afrika, leo imetambulisha huduma yake mpya ya ‘Taxify Bajaj’ ambayo ni App maalum kwa ajili ya Usafiri wa Bajaj huku wakiichagua Dar es salaam kuwa jiji la kwanza katika uzinduzi wa huduma hii.

Kupitia uzinduzi wa huduma hiyo, Taxify sasa imepiga hatua zaidi katika jitihada zake za kupunguza msongamamo jijini Dar es Salaam, mara baada ya uzinduzi wa App yake maalum kwa ajili ya usafiri wa teksi miezi miwili iliyopita.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo jijini Dar es Salaam, Meneja wa Maendeleo Taxify, Kanda ya Afrika Mashariki, Shivachi Muleji alisema, ‘Taxify Bajaj’ ni App mpya ya Taxify jijini Dar es Salaam ambayo inaunganisha watumiaji wa usafiri wa Bajaji na madereva ndani ya dakika chache.

"Tunafurahi sana kuanzisha huduma hii kwa mara ya kwanza kabisa jijini Dar es Salaam pia ni tumaini letu kuwa huduma hii itapokelewa vyema. Tunaamini kwamba huduma hii inaendana na utamaduni wa wakazi wa jiji hili na kwamba itatoa urahisi wa watu kuchagua usafiri anaoutaka kwa gharama nafuu pindi mtu anapotaka kufanya safari zake za mjini”

Shivachi Muleji, Meneja Maendeleo wa Taxify, Kanda ya Afrika Mashariki akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya 'Taxify Bajaji' mwishoni mwa juma. Application hiyo ni maalum kwa ajili ya kurahisisha usafiri wa Bajaj kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam. Taxify sasa inapiga hatua nyingine katika kuleta suluhisho la usafiri hapa jijini, baada ya uzinduzi wa App yake kwa ajili ya magari miezi miwili iliyopita jijini Dar es salaam. Gharama za Taxify Bajaji kwa kipindi hiki zitakuwa kama ifuatavyo ya kuanzia TZS; Sh 750, TZS 350 kwa kila kilometa moja. TZS 75 kwa dakika huku bei ya kiwango cha chini ikiwa ni Shilingi 2000

Shivachi Muleji, Meneja Maendeleo wa Taxify, Kanda ya Afrika Mashariki akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya 'Taxify Bajaji' mwishoni mwa juma. Application hiyo ni maalum kwa ajili ya kurahisisha usafiri wa Bajaj kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam. Taxify sasa inapiga hatua nyingine katika kuleta suluhisho la usafiri hapa jijini, baada ya uzinduzi wa App yake kwa ajili ya magari miezi miwili iliyopita jijini Dar es salaam. Kushoto ni Meneja Uendeshaji wa Taxify Tanzania, Remmy Eseka.
Fenelisti Simon Metumba, Dereva wa Usafiri wa Bajaji jijini Dar es salaam akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mwishoni mwa juma wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma mpya ya 'Taxify Bajaji'. App maalum iliyozinduliwa na kwa ajili ya kurahisisha usafiri wa Bajaj kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam. Taxify sasa inapiga hatua nyingine katika kuleta suluhisho la usafiri jijini Dar es Salaam, baada ya uzinduzi wa App yake maalum kwa ajili ya magari miezi miwili iliyopita jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...