*Wizara ya Mambo ya Ndani yaelezea kinachoendelea
*Rais Magufuli aagiza waliohusika wachukuliwe hatua
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
WIZARA
ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imewahakikishia Watanzania kuwa uchunguzi wa
kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Aqwilina
Akwiline aliyeuawa kwa kupigwa risasi utafanyika kwa haraka na weledi
mkubwa na kufafanua waliohusika na kifo hicho kwa namna yoyote ile hatua
kali za kisheria zitachukuliwa.
Imesema tukio
la mwanafunzi huyo limewasikitisha Watanzania wote na Wizara hiyo
imeanza kufanya uchunguzi ili kupata taarifa sahihi za tukio la kupigwa
risasi mwanafunzi huyo na kwamba iwe kwa ofisa wa polisi au viongozi wa
kisiasa wakithibitika kuhusika watachukuliwa hatua ili iwe fundisho kwa
wengine kwani Serikali haipo tayari kuona raia hata mmona anapoteza
maisha.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam
na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Yusufu Masaun wakati
anaelezea tukio la kifo cha mwanafunzi Aqwilina aliyekuwa anasoma
mwaka wa kwanza katika chuo hicho.
UCHUNGUZI WAANZA
Akizungumzia
hatua ambazo zimeanza kuchukuliwa kutokana na mauaji ya mwanafunzio
huo, Masaun amesema tayari vyombo vya ulinzi na usalama vimenza
kuchunguza tukio hilo ili kubaini waliohusika na kwa sasa ni mapema
kusema fulani ndio amehusika moja kwa moja.
Amesema
Serikali imesikitishwa na kifo hicho lakini uchunguzi unaendelea na
atakayebainika kuhusika kwa namna yoyote hatua za kisheria
zitachukuliwa.
"Tutahakikisha hatua
zinachukuliwa haraka kwa waliohusika na hakuna ambaye ataachwa iwe ofisa
wa polisi au viongozi wa vyama vya siasa.Kiujumla matatizo ya uvunjifu
wa amani lazima yachukuliwe hatua na waliohusika kwenye hilo nalo lazima
wachukuliwe hatua kali,"amesema Masauni.
Amefafanua wapo viongozi wa kisiasa ambao walikuwa wanatoa kauli za kuashiria uvunjifu wa amani ambao nao lazima wachunguzwe.
Amesema
lengo la uchunguzi huo ni kupata taarifa sahihi ili asije kuoonekana
hatua zimechukuliwa bila kufanyika uchunguzi, hivyo wameanza na
uchunguzi ambao anaamini utakamilika kwa haraka.
Ameongeza
uchunguzi huo utafanyika kwa weledi na umakini wa hali ya juu ili
kuhakikisha haki inatendeka huku akieleza kwa sasa hawawezi kusema
wamekamatwa watu wangapi kutokana na tukio hilo ila uchunguzi
ukikamilika watatoa taarifa kwa umma hatua zinazofuata.
Waziri wa Mambo ya Ndani Nchi, Hamad Masauni akizungumza na waandishi wa abari mapema leo mchana jijin Dar,kuhusu kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Aqwilina Akwiline aliyeuawa kwa kupigwa risasi Mkwajuni,Kinondoni jijini Dar.Masauni amewahakikishia Watanzania kuwa uchunguzi wa kifo utafanyika kwa haraka na weledi mkubwa na kufafanua waliohusika na kifo hicho kwa namna yoyote ile hatua kali za kisheria zitachukuliwa. Picha Michuzi Jr.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...