Na Jumbe Ismailly -HANANG    


WANANCHI  300 wa Kitongoji cha Kinachere,kata ya Sirop,tarafa ya Simbay,wilayani Hanang,Mkoani Manyara kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Hanang wameanza ujenzi wa kisima na tanki la kuhifadhia maji ya mvua ili waweze kuondokana na adha ya kufuata huduma hiyo  umbali wa zaidi ya mita 400 kutoka kwenye makazi yao.
Mwenyekiti mstaafu wa Kijiji hicho,Peter Qwendo alisema mradi huo utakapokamilika unatarajia kugharimu zaidi ya shilingi milioni 49 na kwamba kati ya kiasi hicho cha fedha nguvu za wananchi ni asilimia kumi ya gharama za mradi huo kwa kufanyakazi ya kukusanya mawe,mchanga,kokoto,kuchota maji na kumwagilia.
Aidha Qwendo ambaye pia ni mmoja wa watu waliokwenda nchini Kenya kupata mafunzo juu ya usimamizi wa shughuli hiyo,alisema wananchi hao wanaoishi katika kaya 107 wamekuwa wakiifuata huduma hiyo katika Kitongoji cha Ghata kilichopo umbali wa takribani kilomita 14 kwenda na kurudi.
ananchi wa Kitongoji cha Kinachere,kata ya Sirop,Tarafa ya Simbay wakifanya kazi za mikono kuhakikisha mradi huo unakamilika katika kipindi cha mwezi mmoja na kuanza kunufaika na huduma ya maji safi na salama.
bunge wa Jimbo la Hanang,Dk.Mary Nagu akiungana na wananchi wa Kitongoji cha Kinachere kufanyakazi za kukusanya na kusomba mchanga wa kujengea kisima pamoja na tenki la kuhifadhia maji ya mvua na kuahidi kuchangia lori tano za mchanga.
mafundi wa kujenga kisima wakiendelea na kazi ya kusuka nondo za kisima kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wake katika kipindi cha mwezi mmoja.(Picha zote Na Jumbe Ismailly)
Ni Mbunge wa Jimbo la Hanang,Mkoani Manyara,Dk.Mary Nagu(wa kwanza kutoka kushoto) akipata maelezo mafupi ya mradi wa ujenzi wa kisima na tenki la kuhifadhia maji ya mvua kutoka kwa msimamizi wa mradi huo,Apolei Wilbrod.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...