Na John Nditi, Gairo
WANAWAKE wajawazito 2,600  sawa na asilimia 27 kati ya 9,577 waliojifungulia  zahanati na vituo vya afya  kwa mwaka 2017 katika halmashauri ya wilaya ya Gairo , mkoani Morogoro walibainika  kuwa  chini  umri wa  miaka 20.

Hali hiyo ilisababisha  kujitokeza  kwa vifo  vitokanavyo na uzazi pingamizi unaochagiwa na uchungu mkali,  kutokwa damu nyingi baada ya kujifungua  na kifafa cha mimba.

Mratibu wa Afya  ya Mama na Mtoto wa wilaya ya Gairo, Edifonzia Mhafigwa alisema hayo   wakati akiwasilisha taarifa katika   mkutano wa kujadili utoaji wa elimu kuhusu kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi kwenye   siku ya  Utepe Mweupe ambayo  kimkoa ilifanyika  katika  kata ya Ukwamani , wilayani humo.

Mbali na changamoto hiyo, wanawake wajawazito waliojifungulia kwa wakunga wa jadi  kwa mwaka 2017 walifikia 1,270 , waliojifungulia njiani  ni 108 , waliojifungulia nyumbani ni 180 na kwenye  Zahanati walikuwa ni 3,482.
 Katibu Tawala wa wilaya ya Gairo, mkoani Morogoro, Adam Bibangamba ( aliyesimama) akitoa hotuba yake ya  ufunguzi wa mjadala wa elimu  juu ya  njia ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pingamizi kwa  wanawake wajawazito  na kupinga mimba za utotoni  wakati wa siku ya utepe mweupe iliyofanyika  kata ya Ukwamani , wilayani humo. ( Picha na John Nditi).
Mkazi wa  Kata ya Ukwamani , wilaya ya Gairo akichangia mada
  Baadhi ya wananchi  wa kata ya Ukwamani , wilaya ya Gairo, mkoani Morogoro wakisiiliza na kusoma vipeperushi vya  elimu  ya  njia ya kupunguza vifo vitokanavyo  na uzazi vya akina mama wajawazito na kupinga mimba za utotoni, wakati wa mjadala wa uelimisghaji jamiii  siku ya utepe mweupe iliyofanyika  kwenye kata hiyo.
Wazee wa  kata ya Ukwamani, wilaya ya Gairo, mkoani Morogoro ( mstari wa mbele ) wakiwasikiliza wataalamu wa afya ( hawapo pichani) wakati wa utoaji wa elimu  ya  njia ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pingamizi kwa  akina mama wajawazito na kupinga vita  kujifungulia kwa wakunga wa jadi na  mimba za utotoni, wakati wa siku ya utepe mweupe iliyofanyika  kwenye kata hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...