Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) ameishukuru Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DfID) kwa kuwa moja kati ya wadau wa maendeleo nchini.

Mhe. Mkuchika amesema hayo leo katika kikao na ujumbe kutoka Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DfID) kilichofanyika ofisini kwake jijini Dar es Salaam.Ninapenda kuishukuru DfID pamoja na Serikali ya Uingereza kwa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania ili kuleta maendeleo kwa Watanzania wote.

Mhe. Mkuchika amesema DfID kama moja ya washirika wa maendeleo wamechangia kwa kiasi kikubwa jitihada za serikali za kupambana na rushwa, na moja ya matokeo yake ni kuongeza uwajibikaji katika utoaji huduma kwa wananchi na kuondosha rushwa kupungua.

Mhe. Mkuchika ameuhakikishia ujumbe wa DfID kuwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora iko tayari muda wowote kushirikiana na DfID katika kuleta maendeleo.Kiongozi wa DfID nchini, Bi. Beth Arthy ameahidi kuendeleza ushirikiano katika utekelezaji wa masuala mbalimbali ya maendeleo nchini.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) akiwa katika kikao na ujumbe kutoka Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DfID) nchini Tanzania, (hawapo pichani) ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) akiwa katika kikao na ujumbe kutoka Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DfID) nchini Tanzania, ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. 
Kiongozi wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DfID) nchini Tanzania, Bi. Beth Arthy akizungumza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) hayupo pichani wakati wa kikao leo jijini Dar es Salaam.
Kiongozi wa ujumbe kutoka Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DfID) nchini Tanzania, Bw. Nicholas Leader akiwa katika kikao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) hayupo pichani, ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...